WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MIAKA MITANO HATARINI KUFA KWA KUKOSA DAMU
Kamanda wa jeshi la zima
 moto na uokoaji mkoani Pwani, mrakibu msaidizi,Goodluck Zerote 
,akichangia damu ,katika zoezi lililoendeshwa na jeshi hilo ,kuchangia 
damu hospital ya rufaa ya Tumbi.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
………………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
WATOTO chini ya umri wa miaka mitano mkoani Pwani wako kwenye hatari ya kupoteza maisha kutokana na ukosefu wa damu.
Hayo yalielezwa na afisa
 muuguzi wa wa kitengo cha damu salama hosptali ya rufaa ya Tumbi 
,Elisia Towo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya zoezi
 la utoaji damu kwa hiari lililokuwa likiendeshwa na jeshi la zima moto 
na uokoaji mkoani hapo.
Alisema watoto wenye 
umri huo wamekuwa wakiongoza kwa kukosa damu kutokana kuugua ugonjwa wa 
malaria lakini pia kucheleweshwa kuwahishwa hospitali mapema.
“Tumekuwa 
tukiwahamasisha wazazi katika mihadhara mbalimbali kuhakikisha 
wanawawahisha watoto hosptali pindi wanapoona dalili ya  homa ama 
malaria badala ya kuwaleta wakiwa wameshachoka na ugonjwa”, alisema 
Towo.
Alieleza kuwa kundi 
jingine lililo hatarini ni wakina mama wajawazito ambao nao wamekuwa 
wakipata tatizo la ukosefu wa damu ama wakihitaji kufanyiwa upasuaji .
Towo amesema watu wengine ni majeruhi wa ajali ambao hawatabiriki kwani ajali hutokea bila ya kuwa na taarifa.
Muuguzi huyo alisema 
kutokana na mahitaji hayo hosptali ya rufaa ya Tumbi inahitaji damu 
nyingi zaidi ambapo kwa sasa iliyopo  ni unit 25 ambayo ni ndogo 
ikilinganishwa na matukio ya mara kwa mara ya ajali.
“Kwa siku tunakusanya 
unit 12 hadi 20 na mahitaji yetu kwa mwezi ni kuanzia unit 250 hadi 300,
 bado damu haitoshi, nawaomba wananchi wa mkoa wa Pwani wajitokeze 
kuchangia damu kwa hiari ili waweze kuokoa maisha ya watanzania wenzetu 
wanaohitaji damu”, alisema Towo.
Afisa uhusiano wa  jeshi
 la zima moto na uokoaji SGT Harrison Mkonyi alisema zoezi hilo ni 
endelevu na kuwa lengo ni kuhakikisha jeshi hilo linatimiza kauli mbiu 
yake ya kuokoa maisha na mali kwa vitendo.
Kamanda wa jeshi la 
zimamoto na uokoaji mkoani Pwani  Mrakibu msaidizi Gudluck Zerote 
,alisema hii ni mara ya kwanza kwa jeshi hilo mkoani humo kuchangia 
damu.
Kamanda Zerote alisema 
kutokana na kuwa kwa mara ya kwanza  wamechangia damu hosptali ya Tumbi 
unit 12, na kuwa watachangia  baada ya miezi mitatu.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni