MAJALIWA AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA JICA JIJINI NAIROBI
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa 
akizungumza na Makamu wa Rais wa Shirika la Kimataifa  la Misaada la 
Japan,(JICA) Bw. Hiruchi Kato  (kulia kwake) na ujumbe wake , jijini 
Nairobi Agosti 26, 2016 ambako  anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa sita 
Wa Tokyo International Conference on Africa Development (TICAD). Kushoto
 kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Japan Mathias Chikawe. (Picha na 
Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………………………..
*Kampuni Chiyoda kufundisha Watanzania masuala ya gesi
*JICA kusaidia ujenzi wa miundombinu Dodoma
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa 
amewasili Nairobi, Kenya kuhudhuria Mkutano wa Mkuu wa Sita wa Wakuu wa 
Nchi wa TICAD (TICAD VI) utakaofanyika Agosti 27 -28, mwaka huu. Waziri 
Mkuu anahudhudia mkutano huo kwa niaba ya Rais, Dk. John Pombe Magufuli.
Leo asubuhi (Ijumaa, Agosti 26, 
2016) Waziri Mkuu amekutana na viongozi wakuu mbalimbali wa makampuni ya
 kibiashara kutoka Japan ambao wamekuja kuhudhuria mkutano huo.
Waziri Mkuu amekutana na Makamu wa
 Rais wa Kampuni ya Chiyoda Corporation, Bw. Tadashi Izawa ambapo katika
 mazungumzo yao, pamoja na kuangalia fursa nyingine katika sekta ya gesi
 Tanzania, kampuni hiyo imekubali kutoa mafunzo ya kujenga uwezo wa 
wataalamu kwa sekta ya gesi hususan usindikaji wa gesi kwa ajili ya 
kusafirisha nje ya nchi (Liquefied Natural Gas).
Bw. Izawa amemweleza Waziri Mkuu 
kwamba wamefurahiswa na taarifa za ugunduzi wa gesi ya Helium hapa 
nchini Tanzania na kwamba kampuni yake ina teknolojia na uzoefu wa muda 
mrefu katika kutekeleza miradi ya gesi (Gas value Chain Planning and Execution).
“Tunao uzoefu wa muda mrefu, pia 
tunazo teknolojia za kuendeleza sekta ya gesi ikiwemo Helium kwa mfano 
ujuzi wa kutenganisha gesi asilia na helium (Separation of Natural Gas 
and Helium). Tumetekeleza miradi ya namna hii nchini Qatar ambayo kwa 
sasa ni ya pili kwa uzalishaji wa gesi hiyo duniani ikitanguliwa na 
Marekani,” amesema.
Amesema mafunzo hayo yatafanyika 
kuanzia mwakani na yatalenga vijana wasiopungua 10 kutoka Tanzania ambao
 wamehitimu shahada za uhandisi kwani wameshafanya hivyo kwa vijana 
wanane kutoka Msumbiji.
Waziri Mkuu alimshukuru Vw. Izawa 
kwa mpango wao wa mafunzo kwa vijana wa Kitanzania lakini akamtaka pia 
waangalie uwezekano wa kuwasaidia vijana wanaotoka maeneo husika yenye 
gesi ili wapatiwe mafunzo ambayo yatawawezesha kumudu baadhi ya kazi 
kwenye viwanda vya kusindika gesi.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu 
amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Shirika la Misaada 
ya Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Hiroshi Kato na kujadiliana mambo 
kadhaa yakiwemo ya nishati na miundombinu.
Katika mazungumzo hayo, Bw. Kato 
alimweleza Waziri Mkuu nia ya shirika hilo kuendelea kusaidia miradi 
mbalimbali ya kilimo hapa nchini na hasa katika sekta za afya, maji, 
kilimo na miundombinu ambazo imekuwa ikijihusisha nazo kwa muda mrefu 
sasa.
Waziri Mkuu alimshukuru kwa 
ushiriki wa shirika hilo kwenye miradi ya nishati ya Kinyerezi na 
akamtaka aendelee kuisaidia Serikali ya Tanzania inainginia kwenye awamu
 ya tatu ya Kinyerezi (Kinyerezi III).
Katika hatua nyingine, Balozi wa 
Tanzania nchini Japan, Mathias Chikawe alimwoba makamu wa Rais hyo 
waangalie uwezekano wa kuwekeza kwenye sekta za nishati na miundombinu 
ya mkoa Dodoma hasa katika kipindi ambacho Serkali imeamua kuhamia huko.
“Tunaomba muangalie sana suala la 
kuendeleza nishati ya umeme kwani nchi yetu imeamua kuwa nchi ya 
viwanda. Tutahitaji kuwa na umeme wa kutosha kuendesha viwanda vya 
usindikaji bidhaa zetu, lakini pia si mbaya mkiangalia suala la 
kuboresha miundombinu ya barabara na usafirishaji katika mji wa Dodoma,”
 amesema.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni