Kilele Maadhimisho Siku ya vijana Kitaifa kufanyika Mkoani Simiyu.
(Picha na Frank Mvungi-Maelezo
………………………………………………………………………………………………………………..
Frank Mvungi-Maelezo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi siku 
ya Kilele cha maadhimisho ya siku ya Vijana Kitaifa yatakayofanyika 
Mkoani Simiyu Oktoba 14 mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini 
Dar es salaam na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na 
Wenye Ulemavu Mhe. Antony Mavunde wakati wa mkutano na waandishi wa 
Habari.
Mhe Mavunde amebainisha kuwa 
Kauli mbiu ya Siku ya Vijana mwaka huu ni “Tokomeza umasikini kwa 
uzalishaji endelevu na matumizi yenye tija”.
Akifafanua kuhusu kauli mbiu hiyo
 Mhe. Mavunde amesema lengo la kauli mbiu hii ni kuzihimiza nchi 
wanachama wa umoja wa mataifa kushirikisha kikamilifu Vijana katika 
shughuli za uzalishaji na kuhakikisha kuwa panakuwepo na matumizi sahihi
 ya rasilimali za nchi kama vile ardhi,maji,madini na Nishati ili 
kufikia shabaha ya kuwa na maendeleo endelevu ifikapo 20130.
Akizungumzia maadhimisho hayo 
Kitaifa Mhe . Mavunde amesema kuwa vijana watapata fursa ya kushiriki 
shughuli mbalimbali kama makongamano,matamasha,michezo,maonnyesho ya 
Kazi za Vijana,Shughuli za kujitolea na maandamano ya amani.
“Tanzania tutasherekea siku ya 
Vijana Duniani Kitaifa kuanzia tarehe 8/10/2016 na kilele kitakuwa 
tarehe 14/10/2016 Mkoani Simiyu ambapo Sherehe hii itaenda sambamba na 
Maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius 
Kambarage Nyerere, Wiki ya Vijana Kitaifa na kilele cha mbio za Mwenge 
wa Uhuru mwaka 2016.” Alisisitiza Mhe. Mavunde.
Wazo la kuwa na siku ya Vijana 
Duniani lilitolewa katika Mkutano wa Vijana wa Kimataifa mwaka 1991 
Mjini Vienna Australia kwa madhumuni ya kutafuta njia ya kuchangisha 
fedha za kusaidia mifuko ya Taifa ya Vijana ambapo mwaka 2000 nchi 
wanachama wa Umoja wa Mataifa ikiwemo Tanzania zilianza kuadhimisha siku
 ya Vijana Duniani kulingana na mazingira yake kwa kuzingatia kauli mbiu
 ambayo huandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni