Watanzania washauriwa kutumia Lugha ya Kiswahili kuutangaza Utamaduni
Mkurugezi Msaidizi Lugha Bibi
Hajjat Shani Kitogo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye
Dira Tanzania (UWARIDI) katika ukumbi wa Nafasi Arts Space Jijini Dar es
Salaam Agosti 25,2016.
Rais wa Umoja wa Waandishi wa
Riwaya wenye Dira Tanzania (UWARIDI) Bw. Hussein Tuwa akitoa neno wakati
wa uzinduzi wa Umoja huo katika ukumbi wa Nafasi Arts Space Jijini Dar
es Salaam Agosti 25,2016.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Waandishi
wa Riwaya wenye Dira Tanzania (UWARIDI) Ibrahim Gama akitoa maelezo kwa
mgeni rasmi kuhusu Umoja wao wakati wa uzinduzi wa Umoja wa huo katika
ukumbi wa Nafasi Arts Space Jijini Dar es Salaam Agosti 25,2016.
Mkurugezi Msaidizi Lugha Bibi
Hajjat Shani Kitogo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
akionesha cheti cha usajili wa Umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye Dira
Tanzania (UWARIDI) mara baada ya kuuzindua umoja huo huo katika ukumbi
wa Nafasi Arts Space Jijini Dar es Salaam Agosti 25,2016.
Baadhi ya wanachama wa Umoja wa
Waandishi wa Riwaya wenye Dira Tanzania (UWARIDI) wakimsikiliza
mwakilishi wa mgeni rasmi Mkurugezi Msaidizi Lugha Bibi Hajjat Shani
Kitogo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo(hayupo
pichani) katika uzinduzi wa umoja huo katika ukumbi wa Nafasi Arts Space
Jijini Dar es Salaam Agosti 25,2016.
Mkurugezi Msaidizi Lugha Bibi
Hajjat Shani Kitogo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo(wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamojja na viongozi na
wajumbe wa kamati kuu ya Umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye Dira
Tanzania (UWARIDI) mara baada ya uzinduzi wa umoja huo katika ukumbi wa
Nafasi Arts Space Jijini Dar es Salaam Agosti 25,2016.
Baadhi ya vitabu vya Riwaya vilivyoandikwa na wanachama wa Umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye Dira Tanzania (UWARIDI).
……………………………………………………………….
Na Raymond Mushumbusi WHUSM
Watanzania wameshauriwa kutumia Lugha ya Kiswahili katika ulimwengu wa uandishi ili kuutangaza Utamaduni wa nchi.
Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es
Salaam na Mkurugezi Msaidizi Lugha Bibi Hajjat Shani Kitogo kutoka
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakati wa uzinduzi wa Umoja
wa Waandishi wa Riwaya wenye Dira Tanzania (UWARIDI).
Mkurugenzi amesema kuwa kwa
kutumia Lugha ya Kiswahili kutasaidia kuendeleza na kuenzi juhudi za
kuenzi na kuendeleza juhudi za watetezi za masuala ya lugha wa masuala
ya Lugha na Utamaduni wa mtanzania.
Ameongeza kuwa Serikali kupitia
Baraza la Kiswahili la Taifa imeandaa kanuni za Sheria ya BAKITA ya
mwaka 1967 inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni ambayo
itatoa majibu ya changamoto zinazowakabili waandishi hapa nchini pamoja
na haki zao katika kuendeleza fani mbalimbali za Lugha.
“Katika azma ya kukuza na
kuendeleza Lugha ya Kiswahili tuige mfano wa Rais wetu Mhe.Dkt John
Pombe Magufuli wa kutumia Lugha ya kiswahili katika hotuba zake
mbalimbali za kitaifa na kimataifa” alisema Bibi. Hajjat Shani.
Kwa upande wake mmoja ya wajumbe
wa kamati kuu Bi. Matilda Sendwa katika risala yao kwa mgeni rasmi
amesema kuwa umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye Dira Tanzania(uwaridi)
wameamua kutafuta njia ya kurudisha, kutetea, kulinda na kuipandisha
heshima yetu kama waandishi na heshima ya kazi zetu zote.
“Tumeamua kutafuta mbinu za kuweza
kuhakikisha kuwa heshima ya kazi zetu zinatambuliwa rasmi kiserikali na
kijamii kwa ujumla kwa kuanzisha umoja wetu ambao utakuwa na sauti
katika kutetea haki za waandishi na kazi zao alisisitiza Bi. Matilda.
umoja wa Waandishi wa Riwaya wenye
Dira Tanzania (uwaridi) umeanzishwa kwa lengo la kuwatetea waandishi wa
Riwaya nchini ili waweze kunufaika na kazi zao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni