VIJANA JIAJIRINI NA KUJITUMA ILI KUJILETEA MAENDELEO
Na Mwashungi Tahir /Rahma Khamis Maelezo-Zanzibar
………………………………….
Vijana nchini wametakiwa kuongeza bidii ya kujituma na kujiajiri wenyewe ili kujiletea maendeleo endelevu.
Hayo yameelezwa na Naibu Katibu 
Wizara ya Vijana Kazi,uwezeshaji Wazee,Vijana wanawake na Watoto Maua 
Makame Rajab wakati akifungua Kongamano la vijana ikiwa ni shamra shamra
 ya Siku ya Vijana duniani huko katika Ukumbi wa Haileselas mjini 
Zanzibar.
Amesema kujiajiri ni njia nzuri ya
 kupambana na umaskini katika jamii na kuepukana na tabia ya kutegemea 
Serikali pekee kuwaajiri Vijana hao.
Maua amefafanua kwamba ili Vijana 
waweze kujiajiri kwa wepesi ni vyema Vijana hao wakashirikiana na wenzao
 kujiunga katika vikundi vya ushirika.
Kwa kufanya hivyo kutawasaidia 
Vijana hao kujikwamua katika dimbwi la umaskini na kuepukana na vitendo 
viovu ambavyo vijana wengi siku hizi hujiingiza katika makundi maovu 
ikiwemo utumiaji wa madawa ya kulevya na udhalilishaji wa kijinsia.
Aidha Naibu huyo amewatia moyo 
Vijana hao na kuwaambia kuwa hakuna lisilowezekana pale watakapojipanga 
kupambana na changamoto za uhaba wa ajira kwa ktumia fursa zilizotolewa 
na Serikali ikiwemo mikopo ya kujiwezesha kimaisha.
Akitoa mada katika Kongamano hilo 
Naibu Waziri wa kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi Zanzibar,Lulu Msham 
amesisitiza Vijana hao kukubali kijiunga katika ushirika na kujiendeleza
 katika vikundi ili kuepukana na tabia ya ombaomba.
 “Vijana   tujitambua na tujuwe 
wajibu wetu kwa kujijengea maadili mema katika jamii na tujiepushe na 
kujiingiza  katika vitendo vya uvunjifu wa Amani kwani tukifanya hivyo 
tutajiondeshea uaminifu Nchini,”alisema naibu waziri .
Aidha ametoa wito kwa vijana 
kuzichangamkia fursa za kugombea nafasi za uongozi na kujitokeza kwa 
wingi hasa wanawake ambao bado wapo nyuma kiuongozi.
Akifunga Kongamano hilo la siku 
moja Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Idrisa Kitwana Mustafa amewataka 
vijana kutafuta elimu na kuwa na maadili mema na kuweka ushirikiano 
katika kazi zao za kila siku.
Maadhimisho ya Siku ya Vijana 
kimataifa yanatarajiwa kufanyika kesho katika Uwanja wa Mnara wa Kisonge
 ambapo kauli ya mwaka huu  kuelekea 2030 Tokomeza Umaskini kwa 
Uzalishaji Endelevu na Matumizi yenye Tija.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni