Msanii Nigeria atoa msaada katika Kituo cha Kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, Kigamboni Community Center
Mwanzilishi wa Kampuni ya 
Mahusiano ya Umma, LAS Consultancy Bi. Salha Kibwana  akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu ziara ya msanii Omo Alhaji, 
Jagabana maarufu YCEE (hayupo pichani) leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka 
kulia ni Meneja Miradi wa Tinny Entertainment Oladaro Pratt na 
Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea watoto cha Kigamboni Community Center 
Mbwana Msangule.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Tinny 
Entertainment kutoka Nigeria Arokodare Timilehin akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani kuhusu ziara ya msanii Omo Alhaji, 
Jagabana maarufu YCEE (wa tatu kutoka kushoto) leo Jijini Dar es 
Salaam.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea watoto cha 
Kigamboni Community Center Mbwana Msangule na Meneja Miradi wa Tinny 
Entertainment Oladaro Pratt.
Msanii Omo Alhaji, Jagabana 
maarufu YCEE kutoka Nigeria akizungumza na waandishi wa habari kuhusu 
ziara yake katika Vyombo vya Habari inayoratibiwa na Kampuni ya Uhusiano
 wa Umma ya LAS Consultancy ya Jijini Dar es Salaam leo.Kutoka kushoto 
ni Mwanzilishi wa Kampuni ya LAS Consultancy Bi. Salha Kibwana, 
Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea watoto cha Kigamboni Community Center 
Mbwana Msangule na Meneja Miradi wa Tinny Entertainment Oladaro Pratt.
 Baadhi ya waandishi wa habari 
wakifuatilia mkutano baina ya uongozi wa LAS Consultancy walipokuwa 
wakimtambulisha msanii kutoka Nigeria Omo Alhaji, Jagabana maarufu YCEE 
ambaye yupo nchini kwa ajili ya ziara ya kutembelea Vyombo vya Habari.
Msanii Omo Alhaji, Jagabana 
maarufu YCEE kutoka Nigeria akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya 
shilingi milioni moja kwa Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea watoto cha 
Kigamboni Community Center Mbwana Msangule(kushoto) leo Jijini Dar es 
Salaam Katikati ni Meneja Miradi wa Tinny Entertainment Oladaro 
Pratt.Msanii hyo yupo nchini kufuatia ziara yake kwa Vyombo vya Habari 
inayoratibiwa na Kampuni ya Mahusiano ya Umma ya LAS Consultancy.
Picha na Frank Shija, MAELEZO.
……………………………………………………………………..
Na Sheila Simba,Maelezo
Msanii wa muziki kutoka nchini 
Nigeria Omo Alhaji,Jagabana maarufu YCEE,ametoa msaada wa shilling 
million 1,kwa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu 
cha Kigamboni Community Center(KCC).
Akizungumza katika ukumbi wa Idara
 ya Habari, Maelezo leo jijini Dar es salaam mratibu wa ujio wa msanii 
huyo bi Salha Kibwana amesema kuwa msanii YCEE ametoa msaaada huo katika
 kituo hicho kwa lengo la kusaidia watoto hao ili kujipatia mahitaji 
maalum ya kila siku wawapo kituoni hapo.
“Ametoa msaada huo kutokana na 
faaida anayopata katika kazi zake usanii ili kukuza vipaji na kujenga 
upatikanaji wa elimu wa elimu kwa jamii hasa ya watoto wanaoishi katika 
mazingira hatarishi,”alisema Salha
Akizungumza baada ya kupokea 
msaada huo Mkurugenzi wa kituo hicho Mbwana Msangule,amesema kuwa kituo 
chake kinalea watoto hao ili kuwasaidia kuondokana na maisha magumu 
yanayowakabili.
“msaada huu utasaidia sana 
kwasababu kituo kina watoto 14 wanaoishi kituoni hapo na wengine 
wanakuja na kurudi makwao,na nashukuru sana kwa msaada huu kwani ni 
sanii wa kwanza  kutoka msaada,nawaomba pia wasanii wa ndani kijitokeza 
kutoa msaada”alisema Mbwana
Kwa upande msanii huyo amesema 
kuwa amekuja kutembelea Tanzania ili kujifunza na kuonana na wasanii 
wengine wakubwa wa Tanzania huku akiwataja Diamond na Ali Kiba,ameongeza
 kuwa amefurahi pia kuktana na mashabiki wake ambao amekua wakichati 
kupitia mitanzandao ya kijamii.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni