Alhamisi, 11 Agosti 2016

UVCCM WILAYA YA ARUSHA YAMPONGEZA RAIS DK. MAGUFULI

CCM7777777777,PICHA MOJA
Na Mahmoud Ahmad Arusha
 
BARAZA la umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi ,UVCCM, wilaya ya Arusha, limempongeza rais John Magufuli kwa hatua anazozichukua za  utendaji na kusimamia  ukusanyaji wa mapato ya serikali .
Hayo yameelezwa leo na mwenyekiti wa  UVCCM wilaya ya Arusha, Martini Mnisi, alipokuwa akihutubia kwenye kikao cha baraza kuu la Umoja wa vijana wilaya ya Arusha, lililofanyika ukumbi wa ccm, mkoa na kusisitiza vijana kumuunga mkono rais Magufuli.
Mnisi, amesema hivi karibuni kumetokea upotoshaji kuwa rais anawachukia matajiri na huo ni uongo ambao haufai  kuvumiliwa na Baraza linaukemea ,ukweli ni kwamba rais hawachukii matajiri bali wanaokwepa kulipa kodi hao ndio maadui wa serikali.
Amesema  baraza litatoa ushirikiano kwa Rais ambae ni mwenyekiti wa CCM, taifa kwa hatua za kuwatumbua  watu wasio waadilifu na wazembe ili kurejesha heshima ,hadhi na nidhamu ambayo ilikuwa umetoweka miongoni mwa watumishi wa umma na chama cha mapinduzi.
Mnisi ,akawataka mbunge wa jimbo la Arusha na meya wa jiji la Arusha na kuacha kumtuhumu mkuu wa wilaya kwa madai anawaingilia katika utendaji wao  jambo ambalo sio kweli bali wanapaswa wasome katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili waelewe majukumu na wajibu wa mkuu wa wilaya.
Amesema meya na madiwani wa jiji la Arusha, wameshindwa kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ushuru wa magari katika baadhi ya maeneo na sasa wanaandaa hujuma ya kuipaka matope serikali ionekane utaratibu wa kurejesha  vyanzo vya mapato kutoka kwa wazabuni kuwa hauna manufaa.
Awali akifungua kikao hicho Kamanda wa vijana wa UVCCM, wilaya ya Arusha, Karim Mushi , amewataka vijana ambao ni jeshi la CCM, kujipanga upya ili kutokurejea makosa yaliyosababisha jimbo na kata zake kupotea .
Amesema vijana wanapaswa kutanguliza masilahi ya chama na sio masilahi binafsi  kwa kuwa msingi wa chama cha mapinduzi ni kufanya kazi zake kwa kujitolea hivyo watangulize chama mbele masilahi binafsi baadae.
Mushi, akawataka vijana hao kuhakikisha wanasimamia kwa karibu utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM, na kuhakikisha fedha za rais Magufuli, zinazotolewa kwenye ngazi za mitaa na vijiji zinawafikia walengwa kwa kuwa fedha hizo ni za serikali hivyo zisigeuzwe  kuwa ni mtaji wa kisiasa kwa madiwani wa Arusha.
Amesema inauma sana kuona Cham cha mapinduzi katika jimbo la Arusha kugeuzwa kuwa upinzani ambapo sasa ni sawa na utumwa, na hiyo inatokana na wana ccm kutokukitendea haki chama cha mapinduzi kwenye uchaguzi mkuu .
Munishi, amesema umefika wakati wana ccm kujitafakari upya  kwa kuhakikisha hawarejei kwenye makosa yaliyotokea
 
Kwenye kikao hicho baraza linafanya uchaguzi wa wajumbe watatu wa baraza hilo kujaza nafasi zilizoko wazi sanjari na kujaza nafasi ya mjumbe mmoja kutoka Vijana kwenda wazazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni