UVCCM WILAYA YA ARUSHA YAMPONGEZA RAIS DK. MAGUFULI
Na Mahmoud Ahmad Arusha
BARAZA la umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi ,UVCCM, 
wilaya ya Arusha, limempongeza rais John Magufuli kwa hatua 
anazozichukua za  utendaji na kusimamia  ukusanyaji wa mapato ya 
serikali .
Hayo yameelezwa leo na mwenyekiti wa  UVCCM wilaya ya 
Arusha, Martini Mnisi, alipokuwa akihutubia kwenye kikao cha baraza kuu 
la Umoja wa vijana wilaya ya Arusha, lililofanyika ukumbi wa ccm, mkoa 
na kusisitiza vijana kumuunga mkono rais Magufuli.
Mnisi, amesema hivi karibuni kumetokea upotoshaji kuwa rais
 anawachukia matajiri na huo ni uongo ambao haufai  kuvumiliwa na Baraza
 linaukemea ,ukweli ni kwamba rais hawachukii matajiri bali wanaokwepa 
kulipa kodi hao ndio maadui wa serikali.
Amesema  baraza litatoa ushirikiano kwa Rais ambae ni 
mwenyekiti wa CCM, taifa kwa hatua za kuwatumbua  watu wasio waadilifu 
na wazembe ili kurejesha heshima ,hadhi na nidhamu ambayo ilikuwa 
umetoweka miongoni mwa watumishi wa umma na chama cha mapinduzi.
Mnisi ,akawataka mbunge wa jimbo la Arusha na meya wa jiji 
la Arusha na kuacha kumtuhumu mkuu wa wilaya kwa madai anawaingilia 
katika utendaji wao  jambo ambalo sio kweli bali wanapaswa wasome katiba
 ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili waelewe majukumu na wajibu wa 
mkuu wa wilaya.
Amesema meya na madiwani wa jiji la Arusha, wameshindwa 
kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ushuru wa magari katika baadhi ya 
maeneo na sasa wanaandaa hujuma ya kuipaka matope serikali ionekane 
utaratibu wa kurejesha  vyanzo vya mapato kutoka kwa wazabuni kuwa hauna
 manufaa.
Awali akifungua kikao hicho Kamanda wa vijana wa UVCCM, 
wilaya ya Arusha, Karim Mushi , amewataka vijana ambao ni jeshi la CCM, 
kujipanga upya ili kutokurejea makosa yaliyosababisha jimbo na kata zake
 kupotea .
Amesema vijana wanapaswa kutanguliza masilahi ya chama na 
sio masilahi binafsi  kwa kuwa msingi wa chama cha mapinduzi ni kufanya 
kazi zake kwa kujitolea hivyo watangulize chama mbele masilahi binafsi 
baadae.
Mushi, akawataka vijana hao kuhakikisha wanasimamia kwa 
karibu utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM, na kuhakikisha fedha za 
rais Magufuli, zinazotolewa kwenye ngazi za mitaa na vijiji zinawafikia 
walengwa kwa kuwa fedha hizo ni za serikali hivyo zisigeuzwe  kuwa ni 
mtaji wa kisiasa kwa madiwani wa Arusha.
Amesema inauma sana kuona Cham cha mapinduzi katika jimbo 
la Arusha kugeuzwa kuwa upinzani ambapo sasa ni sawa na utumwa, na hiyo 
inatokana na wana ccm kutokukitendea haki chama cha mapinduzi kwenye 
uchaguzi mkuu .
Munishi, amesema umefika wakati wana ccm kujitafakari upya  kwa kuhakikisha hawarejei kwenye makosa yaliyotokea
Kwenye kikao hicho baraza linafanya uchaguzi wa wajumbe 
watatu wa baraza hilo kujaza nafasi zilizoko wazi sanjari na kujaza 
nafasi ya mjumbe mmoja kutoka Vijana kwenda wazazi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni