DKT.KIGWANGWALLA AWAPA MIEZI SITA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUWA NA THEATRE ZENYE KUFANYA KAZI
Waganga wakuu wa mikoa na wilaya 
wote nchini wametakiwa  kuwa na vyumba vya upasuaji ‘theate’ zenye 
kufanya kazi ipasavyo kwenye vituo vyote vya afya kwenye maeneo yao 
ndani ya miezi 6.
Agizo hilo limetolewa na Naibu 
waziri wa Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Hamis 
Kigwangwalla mara baada ya kutembelea kituo cha afya cha Mwandoya 
kilichopo Meatu mkoani Simiyu kilichopo umbali wa kilometa 60 kutoka 
hospitali ya wilaya ya meatu
“Hawa wa Meatu wenyewe wana kituo 
cha Afya Mwandoya wamekipa uwezo wa kufanya upasuaji kituo 
hiki,Wamenunua vifaa, wameajiri hadi Daktari (MD) kwa ajira ya muda kwa 
ajili ya kufanya kazi pale”.
Aidha, alisema  Kituo hicho 
kimefanya takriban operation 40, zote salama Kwa asilimia 100. 
Wamepunguza msongamano Mwanhuzi na wamepeleka huduma nyeti na za kuokoa 
maisha Karibu zaidi na wananchi, ukizingatia huku hakuna barabara za 
lami na hakuna gari la kubebea wagonjwa (ambulances). 
“Leo nimeamua kuchukua uamuzi wa 
kutoa agizo kali kabisa toka nimeteuliwa. Najua litazua maswali, lakini 
litaokoa maisha ya wanawake wajawazito wa nchi yetu (CEmOC) na wananchi 
wengine, Nitalitetea. Nitalisimamia”alisisitiza dkt.Kigwangwalla.
“Wiki iliyopita nilitembelea 
Manispaa ya Ilala, kwenye vituo vya afya vitatu nilivyotembelea hakukuwa
 na theatre yenye kufanya kazi. Kwa mujibu wa sera ya afya ya Tanzania, 
‘kituo cha afya’ kitakuwa na hadhi hiyo kama kina uwezo wa kufanya 
upasuaji. Vinginevyo hiyo ni zahanati. Mara nyingi watendaji hawa 
wamekuwa wakijificha kwenye kichaka cha ‘hatuna fedha’, wengine wakiomba
 fedha kutoka serikali kuu”. 
Hata hivyo alimuuliza Mkurugenzi wa Ilala, anakusanya 
shilingi ngapi Kwa mwezi, akasema bilioni 6. Nikamuuliza unadhani ni 
shilingi ngapi kuwa na theatre yenye kufanya kazi? Akakosa jibu. Nikampa
 miezi 6 awe na theatre zenye kufanya upasuaji. Naibu waziri huyo anasema jana ametembeleaMkoa wa Shinyanga na Simiyu na kukutana na tatizo hilo hilo alipokuwa Kishapu, Shinyanga na Mwanhuzi, Simiyu.
“Nimesema sababu za kuwa Halmashauri hazina pesa huku zinakusanya mamilioni ambayo wanayatumia bila kuainisha matatizo ya msingi ya wananchi hazikubaliki, Leo iwe mwisho”. Nawaagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini washirikiane na Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya wajue watakavyofanya wahakikishe wanafungua huduma za upasuaji kwenye vituo vyote vya afya nchini ndani ya miezi sita (6).
“Baada ya miezi hiyo sita mimi mwenyewe na timu yangu ya kurugenzi ya ukaguzi na uhakiki ubora wa huduma za afya (inspectorate and quality assurance) tutasambaa nchi nzima kukagua huduma hizi na pale ambapo hatutozikuta tutakishusha hadhi kituo hicho kutoka ngazi ya ‘kituo cha afya’ na kuwa ngazi ya ‘zahanati’ sambamba na kuwashauri wenzetu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwa wakuu hao wa idara wameshindwa kutekeleza majukumu yao na hivyo wawashushe vyeo”. “Nitasimamia uamuzi huu Kwa nguvu zangu zote. Sababu ni kwamba ninajua faida yake. Ninajua Mungu atafurahi, atanibariki”.
Wakati wa Bunge la bajeti wanaharakati wa haki za wanawake na Watoto waliwahamasisha Wabunge wawashughulikie Kwa ajili ya suala hili. Wakawa washawishi wabunge kuwa kwa siku takwimu za vifo vinavyotokana na sababu za uzazi ni sawa na ‘coaster’ moja ipate ajali na iue watu wote! Wabunge waligeuka mbogo. Japokuwa namba hizi zilikuwa zilizidishwa, walifikisha ujumbe kwetu mawaziri. Kwamba lazima tufanye kitu tofauti kwenye eneo hili. Mimi naanza kuchukua hatua. Vifo vitokanavyo na uzazi havikubaliki! Alisema Naibu waziri wa afya.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni