KAMPUNI YA UDALALI YA YONO YAINGIA MKATABA WA KIMATAIFA NA KAMPUNI YA BIDDERS CHOICE YA AFRIKA KUSINI
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kampuni ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scholastika 
Christian Kevela (kushoto), akiwaonesha waandishi wa habari Dar es 
Salaam leo (hawapo pichani), mkataba wa kimataifa walioingia na Kampuni 
ya Bidders Choice ya Afrika Kusini wa ushirikiano kwa ajili ya kufanya 
mnada wa mitambo ya kampuni ya uchimbaji ya Acacia inayomiliki mgodi wa 
dhahabu Bulynhulu uliopo mkoani Shinyanga. Kulia ni Mwenyekiti Mtendaji 
wa Kampuni ya Yono, Stanley Kevela.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Yono, Stanley Kevela (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kampuni ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scholastika 
Christian Kevela (kushoto), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo. Kulia 
ni  Mwenyekiti
 Mtendaji wa Kampuni ya Yono, Stanley Kevela. Nyuma kushoto ni Ofisa wa 
kampuni hiyo, Salome Sabas na kulia ni Abdrew Kevela. 
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI
 ya Udalali ya Yono Auction Mart imeingia mkataba wa ushirikiano na 
Kampuni ya Bidders Choice ya  Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya mnada 
wa mitambo ya kampuni ya uchimbaji ya Acacia inayomiliki mgodi wa 
dhahabu Bulynhulu uliopo mkoani Shinyanga .
Akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Mkurugenzi Mtendaji wa
 Kampuni hiyo, Scholastika Kevela alisema wameingia mkataba huo Agosti 
24 mwaka huu ambapo watafanya minada ya kuuza mitambo ya zamani ya 
kampuni ya  Acacia kwa njia ya mtandaoni.
Alisema
 kampuni ya  Bidders Choice imewapa  tenda ya kufanya minada ya mitambo 
ya zamani ya madini mbalimbali ambayo inatakiwa kutolewa na  kuwekwa 
mipya.
“Hivyo
 tunategemea kwenda kwenye mgodi wa dhahabu Bulynhulu kuangalia ni 
mitambo gani inatakiwa kupigwa mnada ili iwekwe mingine,”alisema Kevela.
Mwenyekiti
 wa Kampuni hiyo,Stanley Kevela alisema kampuni yake ilipata tuzo ya 
ufanyaji kazi kwa ubora ambayo imesaidia nchi ya Afrika Kusini kutoa 
 mkataba huo wa kimataifa ambao haujawahi kufanyika nchini kwa kampuni 
nyingine ya udalali isipokuwa ya Yono.
Alisema
 kutokana na utendaji wao kuwa mzuri hivyo wanatarajia kuanzisha chuo 
cha madalali kitakachosaidia  serikali kukusanya mapato ya kutosha.
“Hiki
 chuo cha madalali kikianzishwa kitaleta maendeleo kwenye jamii yetu na 
jamii wataelewa umuhimu wa kukusanya kodi hivyo taifa litapata mapato 
mengi, alisema Kevela.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni