Wadau wa Michezo washauriwa kuwekeza katika Viwanda.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni,
 Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akizungumza na wadau wa 
Michezoalipokuwa akizindua  uzinduzi wa Channeli mpya za Michezo kutoka 
kampuni ya TING Agosti 28,2016.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni 
Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akijadiliana jambo na Mkurugenzi
 Mtendaji wa  Kampuni ya TING Dkt. Veron Fernandez wakati wa uzinduzi wa
 Channeli mbili za Michezo kutoka Kampuni ya TING Agosti 28,2016.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni 
Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akikata utepe kuashiria  uzindua
  wa Channeli mbili za michezo ambazo ni  TING Michezo HD 1 na TING 
Michezo HD 2 kutoka Kampuni ya TING Agosti 28,2016.
Katibu Mtendaji wa Baraza la 
Michezo la Taifa Bw.Said Kiganja akionesha zawadi ya King’amuzi 
aliyopewa na Kampuni ya TING wakati wa uzinduzi wa Channeli mbili za 
Michezo kutoka Kampuni hiyo Agosti 28,2016.
Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya
 TING Dkt .Veron Fernandez akielezea kuhusu faida za channeli mbili mpya
  za michezo kutoka katika kampuni yake zitakavyosaidia kukuza Michezo 
nchini Agosti 28,2016.
……………………………………………………………………
Na Raymond Mushumbusi – WHUSM
Wadau wa Michezo nchini 
wameshauriwa kujenga viwanda kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya michezo 
ili kuleta maendeleo katika sekta hiyo.
Ushauri huo umetolewa jana na 
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia 
Wambura alipokuwa akizindua  channeli mbili za Michezo za  Kampuni ya 
king’amuzi cha TING.
Naibu Waziri Anastazia  alisema 
kuwa kwa kupitia uwekezaji huo kutasaidia kuinua sekta ya michezo nchini
 pamoja na kuondokana na changa moto ya vifaa vya michezo jezi za 
michezo,mipira na vifaa vinginevyo.  
“Tuunge mkono juhudi za Mhe. Rais 
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kuifanya 
Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kuwekeza katika viwanda 
vitakavyotengeneza vifaa vya michezo” alisema Mhe. Anastazia
Aidha, Naibu Waziri huyo aliongeza
 kuwa kuwepo kwa viwanda hivyo kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa
 vifaa vya michezo nchini kwani vifaa vingi vya vinatoka nje ya Tanzania
 hivyo huuzwa kwa bei ya juu.
Kwa upande wake Mkurugenzi 
Mtendaji wa  Kampuni ya TING Dkt. Veron Frenandes ameishukuru Serikali 
kwa kutoa ushirikiano kwa  wadau mbalimbali wa Michezo nchini katika 
kukuza na kuendeleza sekta  hiyo.
Chaneli za Michezo zilizozinduliwa
 katika Kingamuzi hicho ni  ni TING Michezo HD 1 na TING Michezo HD 2 
ambazo zitakuwa zikionesha michezo mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni