Chama cha Waajiri (ATE) chazindua za Waajiri Bora 2016 jijini Dar leo
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha 
Waajiri Tanzania (ATE), Dk. Aggrey Mlimuka (kushoto), akizungumza na 
waandishi wa habari jijini kuhusu tuzo za Mwajiri Bora 2016 
zinazotarajiwa kutolewa mwezi Disemba mwaka huu.  Hafla hiyo ilifanyika 
katika ofisi za ATE,jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Masoko, 
Mawasiliano na Mradi, Joyce Nangai.
 Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na 
Mradi, wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Joyce Nangai (kushoto) 
akizungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari jijini Dar es 
Salaam leo. Kushoto ni Mkurugenzi
Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka.
Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka.
Baadhi ya waandishi wa habari 
wakirekodi wakati Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk Aggrey Mlimuka 
akizungumza nao kuhusu tuzo za mwaka huu za Waajiri Bora zinazotarajiwa 
kutolewa baadae mwaka huu.
……………………………………………………………………….
Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) 
leo kimezindua Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2016 kutambua Waajiri wenye
 misingi bora ya usimamizi wa nguvu kazi na rasilimali watu  ili 
kuwawezesha kutimiza wajibu wao kwa ajili ya kuongeza uzalishaji 
kibiashara.
Akizungumza kwenye Mkutano na 
Waandishi wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa ATE Dkt. Aggrey Mlimuka 
alisema kwamba lengo kuu la Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka ni kutambua 
wanachama wenye sera nzuri za usimamizi wa rasilimali watu.  
Alisema kuwa kwa miaka kadhaa tuzo
 hiyo imesaidia kuhamasisha wanachama kujikita katika kushughulikia 
masuala ya ajira na usimamizi wa rasilimali watu kama msingi muhimu 
katika kumwezesha mwajiri kuwa na wafanyakazi wenye kukikidhi ushindani,
 wanaojituma na wenye furaha.
Aliongeza kuwa tuzo hiyo ilifuata 
mbinu za kisayansi na kitaalamu ili kuangalia  umuhimu wa Rasilimali 
Watu katika makampuni ya kibiashara kuanzia makampuni  makubwa kwa 
madogo na yale ya kati ili kuinua ujuzi na kuwa na wafanyakazi wenye 
kufanaya kazi kwa kujituma kama njia ya kutoa motisha kwa wafanyakazi 
ambao ndio msingi wa rasilimali watu.
Aliongeza kuwa EYA lilikuwa tukio 
muhimu linalofanywa na ATE kila mwisho wa mwaka tangu mwaka 2005. 
 Alisema kuwa tuzo hiyo imekuwa maarufu hapa nchini katika muktadha wa 
biashara hasa kwa kuhamamasisha makampuni makubwa na madogo na ya ukubwa
 wa kati kuhusu umuhimu wa kuzingatia misingi bora ya kufanya biashara 
nchini.
Aliongeza kuwa tukio hilo la 
kutafuta mshindi limegawanyika katika makundi makuu mawili ambapo 
litaanza na kufanya utafiti kwa kutumia Mshauri Mwelekezi na hatua ya 
pili itakuwa ni hafla ya kutoa tuzo yenyewe kwa washindi ambalo 
litafanyika mwezi Desemba 2016.
“Tukio hili limegawanyika katika 
makundi mawili, ambapo hatua ya kwanza ni kufanya utafiti na hatua ya 
pili ni hafla ya kutoa tuzo kwa washindi,” alisema.
Aliwaomba pia Wanachama kushiriki 
kwa wingi ili kuweza kushindana na waajiri wengine kupitia shughuli 
wanazozifanya. Aliongeza kuwa kwa mwaka huu waajiri wataweza kujifunza 
kupitia kile kinachofanywa na makampuni mengine ili kuhakikisha wanakuwa
 na wafanyakazi wenye wanaojituma na wenye furaha katika kufanya kazi. 
  
Dkt. Mlimuka alisema kuwa Tuzo ya 
Mwajiri Bora wa Mwaka 2016, ilikuwa ya 9 tangu kuanza kwake na kuaongeza
 kuwa tuzo hiyo kwa mwaka huu itakuwa ya tofauti kulinganisha na zile 
zilizotangulia kwa kuwa itahusisha tuzo nyingine mbili mpya mojawapo 
ikipima Ushiriki wa Wafanyakazi ili kujua ni kwa kiasi gani wafanyakazi 
wanajihusisha na kazi wanazofanya, wanajitoa kwa ajili ya waajiri wao, 
na kama wana bidii katika utendaji kazi wao.
Alisema kuwa tuzo nyingine mpya 
ilikuwa ikiangalia umuhimu wa Usimamizi wa Vipaji na Kuviendeleza na 
lengo lake ni kuyawezesha makampuni kuvutia, kutunza, kutoa motisha na 
kuendeleza majhitaji ya wafanya kazi kwa sasa na siku za usoni
“Tumeanzisha tuzo mbili mpya kwa 
mwaka huu ili kuwawezesha waajiri kuboresha mazingira ya biashara 
kuhakikisha wafanyakazi wao wanashiriki kikamilifu katka utendaji kazi 
na hivyo kumwezesha mwajiri kupata na kuvutia waafanyakazi wenye ujuzi 
stahiki kwa manufaa ya sasa na siku za usoni,” alisema Dkt. Mlimuka.
Alisema kuwa tuzo hiyo imekuwa 
ikijikita katika kuangalia maeneo muhimu ya kusimamia Rasilimali Watu 
kama vile Uongozi na Utawala, Usimamizi wa rasilimali watu, Kusaidia na 
Kuwajibika kwa Jamii, Ubora na Uzalishaji, Kushirikisha Watu Wenye 
Ulemavu na Kujali Wafanyakazi.
Akizungumzia kuhusu namana ya 
kushiriki katika tuzo hiyo, Dkt. Mlimuka alishauri wanachama kushiriki 
kwa kujaza dodoso kupitia njia mojawapo kati ya njia tatu ambazo ni kwa 
njia ya umeme (Electronically), kwa njia ya mtandao (Online), au kwa 
kuwasilisha dodoso zilizojazwa kwa mkono.
Alikumbusha kuwa wanachama wwanaopenda kushiriki dodoso kupitia anuani ya: www.eya2016.co.tz
  ili kushiriki katka tuzo hii muhimu sana. Alisema kuwa mwisho wa 
kujaza dodoso za ushiriki itatakuwa Ijumaa tarehe 30 Septemba 2016.
Mwaka jana Tuzo ya Mwajiri Bora wa
 Mwaka ilifanyika kwa mafanikio makubwa ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mhe. 
Kassim M. Majaliwa (MB) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
 Ushiriki uliongezeka kwa 100% kulinganisha na mwaka uliopita na kwa 
mwaka huu tunategemea idadi ya washiriki itaongezeka mara dufu. 
Makampuni mengi yalishiriki katika tuzo hiyo na baadhi ya washiriki 
walishinda tuzo hiyo na kati ya washindi hao alikuwa Tanzania Brewies 
Ltd (TBL), CCBRT, Kilombero Sugar Company, Social Security Regulatory 
Authority, Yakubu & Associates Chambers, Total Tanzania Ltd, TIGO 
Tanzania, CRDB Bank Plc na Geita Gold Mine. Kwa taarifa zaidi kuhusu EYA
 iliyopita tembelea www.eya.oc.tz. Mwaka huu tunategemea kuwa wanachama wengi zaidi watashiriki na wanasubiri tuzo hii kwa shauku kubwa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni