Jumanne, 30 Agosti 2016

MAKABIDHIANO YA OFISI MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA- NIDA


mso1
Dr. Modestus Kipilimba (Kushoto) akimkabidhi ripoti ya utekelezaji mradi wa vitambulisho vya Taifa Bw. Andrew Wilson Massawe aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA wakati wa hafla ya Makabidhiano katika ofisi za  Makao makuu ya NIDA
mso2
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. Andrew Wilson Massawe akizungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa mara baada ya hafla ya makabidhiano
mso3
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba aliketi kushoto na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bw. Andrew Wilson Massawe wakiwa katika  picha ya pamoja na Menejimenti ya NIDA, baada ya hafla fupi ya makabidhiano
mso4
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. Andrew Wilson Massawe akikagua mitambo ya uzalishaji vitambulisho alipotembea kituo cha uchakataji na uzalishaji vitambulisho mara baada ya halfa ya makabidhiano. Kulia ni aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa akishuhudia
mso5
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, akikagua mfumo wa uhifadhi taarifa wakati alipotembelea kituo cha uchakataji taarifa (Data Centre) na kushuhudia mfumo wa kielektroniki unavyoendesha shughuli mbalimbali za uzalishaji na uhifadhi wa taarifa katika kituo hicho
mso6
Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba akifafanua jambo wakati akihitimisha ziara ya makabidhiano katika kituo cha uchakataji na uzalishaji vitambulisho. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA Bw. Andrew Wilson Massawe akiwa ameambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti
…………………………………………………………………………….
Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba leo amekabidhi rasmi ofisi kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu mpya Bw. Andrew Wilson Massawe; aliyeteuliwa hivi karibu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA
Katika Hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA, Dr. Modestus Kipilimba amekabidhi ripoti yenye mjumuisho wa taarifa ya utekelezaji mradi wa Vitambulisho vya Taifa na hatua za utekelezaji
Halfa hiyo ilifuatiwa na ziara fupi ya kutembelea kituo cha uchakataji taarifa na uzalishaji vitambulisho (Data Centre) ambapo mbali na kukagua shughuli za uzalishaji, Bw. Massawe alipata fursa ya kukagua mitambo na ubora wa vitambulisho vinavyozalishwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni