MAKABIDHIANO YA OFISI MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA- NIDA
Dr. Modestus Kipilimba (Kushoto) 
akimkabidhi ripoti ya utekelezaji mradi wa vitambulisho vya Taifa Bw. 
Andrew Wilson Massawe aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA 
wakati wa hafla ya Makabidhiano katika ofisi za  Makao makuu ya NIDA
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. 
Andrew Wilson Massawe akizungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Mamlaka 
ya Vitambulisho vya Taifa mara baada ya hafla ya makabidhiano
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya 
Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba aliketi kushoto na Kaimu 
Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bw. Andrew Wilson Massawe wakiwa katika  picha 
ya pamoja na Menejimenti ya NIDA, baada ya hafla fupi ya makabidhiano
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. 
Andrew Wilson Massawe akikagua mitambo ya uzalishaji vitambulisho 
alipotembea kituo cha uchakataji na uzalishaji vitambulisho mara baada 
ya halfa ya makabidhiano. Kulia ni aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA 
ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa akishuhudia
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, 
akikagua mfumo wa uhifadhi taarifa wakati alipotembelea kituo cha 
uchakataji taarifa (Data Centre) na kushuhudia mfumo wa kielektroniki 
unavyoendesha shughuli mbalimbali za uzalishaji na uhifadhi wa taarifa 
katika kituo hicho
Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu 
NIDA ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dr. 
Modestus Kipilimba akifafanua jambo wakati akihitimisha ziara ya 
makabidhiano katika kituo cha uchakataji na uzalishaji vitambulisho. 
Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA Bw. Andrew Wilson Massawe akiwa 
ameambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti
…………………………………………………………………………….
Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa
 Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa 
Idara ya Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba leo amekabidhi rasmi 
ofisi kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu mpya Bw. Andrew Wilson Massawe; 
aliyeteuliwa hivi karibu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA
Katika Hafla fupi ya makabidhiano 
iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA, Dr. 
Modestus Kipilimba amekabidhi ripoti yenye mjumuisho wa taarifa ya 
utekelezaji mradi wa Vitambulisho vya Taifa na hatua za utekelezaji
Halfa hiyo ilifuatiwa na ziara 
fupi ya kutembelea kituo cha uchakataji taarifa na uzalishaji 
vitambulisho (Data Centre) ambapo mbali na kukagua shughuli za 
uzalishaji, Bw. Massawe alipata fursa ya kukagua mitambo na ubora wa 
vitambulisho vinavyozalishwa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni