Jumatano, 3 Agosti 2016
Tanzania
 inazidi kupiga hatua kila uchwao kwenye masuala mbalimbali hivi 
karibuni ilishuhudiwa kwenye masuala ya Filamu mwanadada Elizabeth 
Michael (Lulu) na Single Mtambalike wakileta ushindi nchini baada ya 
kushinda tuzo za Filamu za African Magic Viewers Choice Awards 2016 
zilizotolewa jijini Lagos, Nigeria., huku kwenye Tasnia ya Muziki 
ikishuhudiwa msanii Alikiba akisaini Mkataba na kampuni kubwa ya Sony 
ambapo kwa bara la Afrika yeye na msanii Davido wa Nigeria ndio wamepata
 fursa hiyo adhimu.
Kwa
 upande wa masuala ya Kiroho imeshuhudiwa kwa kijana Rajai Ayoub 
kushinda katika mashindano ya usomaji wa Qur-an kwa mtindo wa Tajweed 
yaliyo fanyika nchini Iran na kushika namba moja kwa kwa Afrika na namba
 sita kwa Dunia, huku katika kipengele cha uzuri wa Sauti akichukua 
namba moja kwa Dunia nzima.
Halikadhalika
 katika nyanja za Maendeleo Tanzania imezidi kufanya vizuri ambapo 
kijana Selemani Yusuph Kitenge amekuwa miongoni mwa vijana waliotunukiwa
 tuzo za Diploma ya Heshima maarufu kama 'New Leaders For Tommorow 
Diploma' zinazo tolewa na Taasisi ya Crans Montana Forum yenye makao 
makuu yake nchini Monaco na Uswis.
Akizungumza
 na Mtembezi.com Selemani Kitenge ameeleza kuwa moja ya sababu 
zilizopelekea kutunukiwa tuzo hiyo ushiriki wake wa mijadala mbalimbali 
ya masuala ya kimaendeleo katika nchi za Russia, Moroco na Azerbaijan, 
ndipo wadau mbalimbali wakapendekeza jina lake katika tuzo hizo, kwa 
Tanzania ni mara ya kwanza kwa kijana Selemani kutunukiwa tuzo hiyo 
tangu zianzishwe mwaka 2010 ambapo atapata fursa ya kushiriki mikutano 
mbalimbali ya kimataifa itakayo wahusisha viongozi wakubwa wa kidunia, 
ambapo amewataka vijana kutokata tamaa na kuamini katika kile 
wanachokifanya.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni