Jumatano, 3 Agosti 2016

 NA RAYMOND URIO

Tanzania inazidi kupiga hatua kila uchwao kwenye masuala mbalimbali hivi karibuni ilishuhudiwa kwenye masuala ya Filamu mwanadada Elizabeth Michael (Lulu) na Single Mtambalike wakileta ushindi nchini baada ya kushinda tuzo za Filamu za African Magic Viewers Choice Awards 2016 zilizotolewa jijini Lagos, Nigeria., huku kwenye Tasnia ya Muziki ikishuhudiwa msanii Alikiba akisaini Mkataba na kampuni kubwa ya Sony ambapo kwa bara la Afrika yeye na msanii Davido wa Nigeria ndio wamepata fursa hiyo adhimu.Alikiba Sony

Kwa upande wa masuala ya Kiroho imeshuhudiwa kwa kijana Rajai Ayoub kushinda katika mashindano ya usomaji wa Qur-an kwa mtindo wa Tajweed yaliyo fanyika nchini Iran na kushika namba moja kwa kwa Afrika na namba sita kwa Dunia, huku katika kipengele cha uzuri wa Sauti akichukua namba moja kwa Dunia nzima.RAJAI TUZO 2

Halikadhalika katika nyanja za Maendeleo Tanzania imezidi kufanya vizuri ambapo kijana Selemani Yusuph Kitenge amekuwa miongoni mwa vijana waliotunukiwa tuzo za Diploma ya Heshima maarufu kama 'New Leaders For Tommorow Diploma' zinazo tolewa na Taasisi ya Crans Montana Forum yenye makao makuu yake nchini Monaco na Uswis.SELEMANI KITENGE (7)

Akizungumza na Mtembezi.com Selemani Kitenge ameeleza kuwa moja ya sababu zilizopelekea kutunukiwa tuzo hiyo ushiriki wake wa mijadala mbalimbali ya masuala ya kimaendeleo katika nchi za Russia, Moroco na Azerbaijan, ndipo wadau mbalimbali wakapendekeza jina lake katika tuzo hizo, kwa Tanzania ni mara ya kwanza kwa kijana Selemani kutunukiwa tuzo hiyo tangu zianzishwe mwaka 2010 ambapo atapata fursa ya kushiriki mikutano mbalimbali ya kimataifa itakayo wahusisha viongozi wakubwa wa kidunia, ambapo amewataka vijana kutokata tamaa na kuamini katika kile wanachokifanya.SELEMANI KITENGE (9)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni