PROF WANGWE ATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa
 Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Prof Samwel Mwita Wangwe amesema 
kuwa uongozi wa Awamu ya Tano umefanya kazi kubwa katika kuweka maslahi 
ya Taifa mbele ikiwamo kuongezeka kwa bajeti ya maendeleo na kupunguza 
matumizi ya serikali.
Hatua hii imesaidia nchi kusonga 
mbele kupitia uboreshaji wa  utendaji kwa watumishi wa umma na hivyo 
kujenga imani kubwa kwa wananchi juu ya Serikali yao.
Profesa Wangwe ametoa kauli hiyo leo mjini Dar es salaam wakati akitoa tathmini ya uongozi wa Awamu ya Tano.
Amesema kuwa Rais Magufuli katika 
uongozi wake umesaidia  kuokoa fedha nyingi za walipa kodi ambazo 
zilikuwa zikiishia mikononi mwa watu wachache na kuzielekeza katika 
shughuli nyingine za maendeleo.
Profesa Wangwe amewataka wananachi
 kumuunga mkono Rais Magufuli kwenye harakati zake za kupambana na 
matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuwa matokeo yake yatasaidia 
kuijenga Tanzania mpya ambayo kila mwananchi atapata fursa kunufaika na 
rasilimali za nchi.
“Kwa kweli Rais huyu amefanya 
mabadiliko makubwa sana na kwa sasa  nchi imerudi katika hali  nzuri, 
 kwani nchi ilikuwa imefika mahali pabaya na kwa hiyo aliona ni budi 
kuhakikisha Rushwa na Ufisadi vinakomeshwa na kwa hili ameanza vizuri na
 nchi inakwenda katika mwongozo mzuri kwani ameboresha utendaji kazini 
serikalini na kubana matumizi ambayo yamesaidia kuokoa pesa nyingi 
ambayo inatumika katika maendeleo ya nchi hii”aliongeza Profesa Wangwe.
Mbali na hayo Profesa Wangwe 
ameshauri Serikali kuweka mfumo mzuri katika ukusanyaji kodi kwa 
kurasimisha biashara ili mfumo huu wa  EFD utumike kirahisi na pia 
kutengenezwe mazingira mazuri ya biashara kwa kuweka mazingira rahisi ya
 kuandikisha biashara kwani huchukua muda mrefu kwani kwa kufanya hivyo 
kasi ya kurahisisha  utendaji na wafanyabiashara watalipa kodi kwa wingi
 na uchumi utakua.
Pia Profesa Wangwe ametoa ushauri 
kwa vyama vya upinzani kuacha na na maandamano yasiyo na tija na badala 
yake wakae chini na kuzungumza na serikali ilikupata mwafaka na hivyo 
amani iendelee kuchanua katika nchi hii.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni