UVCCM KUINGIA MIKATABA MIPYA NA WAPANGAJI WAKE ARUSHA
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Katibu wa Uvccm mkoa wa Arusha 
Ezekiel Mollel amesema kuwa umoja huo utaendelea na kuingia mikataba 
mipya na wapangaji wake waliondani ya vibanda na si vingine.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati 
akiongea na wanahabari ofisini kwake ambapo alikumbushia siku 14 
walizotoa kwa wapangaji hao wa umoja huo wa vijana kuwa zimeisha na 
yeyote atakaekadi hatua zitachuliwa.
Mollel alisema kimsingi 
wamekubaliana kuingia mkataba mipya na wapangaji wote kwenye vibanda 49 
vinavyomilikiwa na umoja huo kwa wapangaji  kuingia mkataba wa mwaka 
mmoja mmoja.
Akatanabaisha kuwa na wale 
wapangaji waliowapangishia hapo mwanzo nao kuwapangishia waliomo wao 
hawatawatambua na kuanzia mwezi ujao wataanza zoezi la kuingia mikataba 
mipya.
Aliwataka wapangaji hao kufuata 
maelekezo waliokubaliana kwenye kikao chao na wale walipangishia wengine
 watakuwa wamejiondoa wenyewe huku aliendani ndie wataingia nae mkataba 
mpya.
“Hiki kibanda no 46 
tumekubaliana na mpangaji aliekuwepo ambaye tulimfungia kuendelea na 
biashara na huyo na mmliki wa awali sisi hatumtambui kwa teyari 
ameshajilipa mwenyewe”alisema Mollel.
Aidha akizungumzi eneo la 
Barcelona lenye eka mbili ambalo pia linamilikiwa na umoja huo alisema 
kuwa wametangaza zabuni za upangaji wa eneo hilo na atakayeshinda zabuni
 ndio ataendesha eneo hilo.
Nae mwenyekiti wa umoja huo 
mkoani hapa Lengai ole Sabaya alisema kuwa suala la nyumba za umoja huo 
ambayo katibu aliekuwepo huko nyuma Kizigo alijiuzia kwa kiasi cha 3 
milion kwenye eneo la Ngarenaro ataalipeleka ngazi za juu kwa maamuzi 
zaidi.
Wiki mbili zilizopita Uvccm 
mkoani hapa walitoa tamko lao mbele ya waandishi wa habari ambapo 
alikemea vikali mikataba iliyoingia ya upangishaji wa vibanda vya umoja 
huo na kujikuta wakiwa hawana kitu huku fedha zikichuliwa na wapangaji 
wao kwa mikataba minono ya 450,000 huku umoja huo ukiambulia 5000 kwa 
kibanda namba 46 haliiliyopekea kuingia na sera mpya ya mikataba ya 
vibanda hivyo
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni