SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA SEKTA YA UCHUKUZI
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akipata maelezo kuhusu uboreshwaji wa 
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT),kutoka kwa Mkuu wa Chuo hicho 
Prof. Zacharia Mganilwa alipokagua chuo hicho jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akikagua moja ya darasa linalotumika 
kufundishia Marubani wa ndege alipokagua  Chuo cha Taifa cha 
Usafirishaji (NIT), jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akiongea na wanafunzi wanaosoma kozi 
ya udereva alipotembelea Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), jijini 
Dar es Salaam. Kushoto (mwenye tai nyekundu) ni Mkuu wa Chuo hicho Prof.
 Zacharia Mganilwa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akibadilishana uzoefu na makapteni wa 
meli ya Azam aliposafiri na boti hiyo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akiongea na mmoja wa abiria wanaotumia
 usafiri wa boti kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar, na kujionea 
changamoto mbalimbali zinazowakabili abiria hao ambapo ameahidi 
kuzipatia ufumbuzi hivi karibuni.
…………………………………………………………………………….
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali imejidhatiti 
kufanya maboresho makubwa ya kimiundombinu na rasilimali watu katika 
sekta za uchukuzi ili kuiwezesha sekta hiyo kuongeza ajira na kukuza 
uchumi wa nchi.
Prof. Mbarawa amesema hayo mara 
baada ya kukagua Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na kusafiri wa 
boti kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar ikiwa ni mkakati wa kupata 
taarifa sahihi kuhusu hali ilivyo sasa kutoka  kwa abiria na waendeshaji
 wa vyombo vya majini.
Amesema Serikali itaboresha 
Bandari ya Dar es Salaam ili kupunguza urasimu usio wa lazima na 
kuwawezesha abiria na boti kukaguliwa kwa haraka na kuondoka kwa muda 
unaotakiwa.
‘Tutahakikisha kuwa idadi ya 
manahodha na wahandisi wa vyombo vya majini wazalendo inaongezeka ili 
mkakati wa kuboresha usafiri wa majini hapa nchini uwiane na uwepo wa 
wataalam wa uhakika’ amesema Prof. Mbarawa.
Waziri huyo wa Ujenzi, Uchukuzi na
 Mawasiliano amesema Serikali ina mpango wa kujenga meli mpya za kisasa 
katika Ziwa Victoria ili kuhamasisha wasafirishaji katika sekta ya 
usafiri majini kuwa na vyombo vya kisasa na hivyo kupunguza gharama za 
usafiri.
Katika hatua nyingine Prof. 
Mbarawa amekagua Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) ambapo 
amesisitiza kuwa Serikali itaunga mkono juhudi zinazofanywa na Chuo 
hicho katika kutoa mafunzo wa marubani wa ndege ili kuongeza idadi ya 
marubani wazalendo.
‘Mpango wetu wakukunua ndege mpya 
unaendana na kuwezesha Chuo hiki chenye kufundisha marubani ili tuwe na 
marubani wazalendo wa kutosha’ amesisitiza Prof. Mbarawa.
Amewataka wafanyakazi wa Chuo 
hicho kufanya kazi kwa uzalendo, ubunifu na kuzingatia matokeo ili 
kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayokwenda haraka.
Naye Mkuu wa Chuo hicho Profesa 
Zacharia Mganilwa amemhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa chuo hicho 
kitashirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRL), Mamlaka ya Reli ya 
Tanzania na Zambia (TAZARA), Kampuni hodi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) 
katika kupata utaalam wa kisayansi katika mradi wa ujenzi wa reli ya 
kati ya Kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.
Serikali imejipanga kujenga chuo 
cha kisasa cha Usafirishaji kwa kushirikiana na Jamhuri ya Watu wa China
 ikiwa ni mkakati wa kukifanya chuo hicho kuwa chuo mahiri katika upande
 wa Afrika Mashariki na Kati.
Zaidi ya Shilingi trilioni 4 
zimetengwa na Serikali katika bajeti ya mwaka huu ili kuimarisha 
miundombinu ya usafiri wa Angani, barabarani, relini na majini.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni