TaBSA KUWANOWA WACHEZAJI WACHANGA WA MPIRA WA MAGONGO
Dar es Salaam
CHAMA cha mchezo wa magongo nchini
 (TaBSA) kwa kushirikiaa na wadau wa mchezo huo kutoka Marekani 
kimeandaa kambi ya mafunzo ya majaribio kwa wachezaji vijana 
yatakayofanyika Jijini Nairobi Kenya tarehe 2-4 Septemba mwaka huu.
Kambi hiyo ni sehemu ya maandalizi
 ya Tanzania kwa ajili ya michezo ya olimpiki ya inayotarajiwa kufanyika
 mwaka 2020 katika Jiji la Tokyo nchini Japan.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa 
kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa TaSBA, Bw. Alpherio Nchimbi 
alisema mafunzo hayo yatawahusisha wanafunzi kutoka shule za Sekondari 
za Azania, Kibasila, Temeke na Tiger Klub.
Nchimbi aliwataja wanafunzi 5 
waliochaguliwa kuhudhuria mafunzo hayo ni Djeskan Dihonga na Leodgar 
Leonidas (Azania), Nathan Joram na Peter Pius (Kibasila) na Musa Mbugi 
(Temeke) na Abdulwahid Anwar kutoka klabu ya Tiger.
Nchimbi aliwata taratibu za maandalizi za safari hiyo zimeanza ikiwemo kuomba ruhusa kutoka kwa Viongozi wa shule hizo.
“Endapo kijana atafanya vizuri 
katika majaribio haya ni nafasi kwake kupata scholarship ya masomo na 
mafunzo ya mchezo huu nchini Afrika kusini na marekani” alisema Nchimbi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni