Jumatatu, 29 Agosti 2016

Mauzo soko la hisa yashuka kwa asilimia 34


index 
Na Ally Daud-Maelezo
Idadi ya mauzo katika soko la hisa Dar es salaam (DSE) imeshuka kwa asilimia 34 na kufikia shilingi bilioni 2.2 kutoka shilingi bilioni 3.3 wiki iliyopita kutokana na ukubwa wa idadi ya mauzo kushuka.
Katika taarifa iliyotolewa na Afisa Mwandamizi wa Masoko DSE Bi. Mary Kinabo imesema kuwa idadi ya mauzo hayo yameshuka kutokana na kupungua  kwa idadi za hisa zilizouzwa kutoka shilingi milioni 2.2 hadi kufikia shilingi milioni 1.3.
Aidha taarifa hiyo iliongeza kuwa Benki ya CRDB imeendelea kuongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kwa asilimia 41 ikifuatiwa na Soko la hisa DSE ikiwa na asilimia 36 na ya tatu ni Benki ya NMB yenye asilimia 9.
Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa ukubwa wa mtaji wa soko umeshuka kwa asilimia 0.03 na kufikia shilingi trilioni 22.7 kutoka trilioni 23.4 wiki iliyopita na ukubwa wa mtaji wa makampuni ya ndani umeshuka kwa 0.01% na kufika Trilioni 8.3 kutoka trilioni 8.4 wiki iliyopita
Mbali na hayo taarifa hiyo imeeleza kwamba licha ya mauzo kushuka lakini pia viashiria vya soko katika sekta ya viwanda vimeshuka kwa alama imeshuka kwa alama 66.10 baada ya bei za hisa za TBL kushuka kwa 2.13% pamoja na kaunta za  DSE kwa asilimia  na DCB kwa asilimia 14.
Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa viashiria vya soko katika sekta ya huduma za kibiashara wiki hii imebaki kwenye hali yake ya wiki iliyopita baada ya bei za hisa za Swissport kubaki shilingi  3,543.02.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni