Mauzo soko la hisa yashuka kwa asilimia 34
Na Ally Daud-Maelezo
Idadi ya mauzo katika soko la hisa
 Dar es salaam (DSE) imeshuka kwa asilimia 34 na kufikia shilingi 
bilioni 2.2 kutoka shilingi bilioni 3.3 wiki iliyopita kutokana na 
ukubwa wa idadi ya mauzo kushuka.
Katika taarifa iliyotolewa na 
Afisa Mwandamizi wa Masoko DSE Bi. Mary Kinabo imesema kuwa idadi ya 
mauzo hayo yameshuka kutokana na kupungua  kwa idadi za hisa zilizouzwa 
kutoka shilingi milioni 2.2 hadi kufikia shilingi milioni 1.3.
Aidha taarifa hiyo iliongeza kuwa 
Benki ya CRDB imeendelea kuongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na 
kununuliwa kwa asilimia 41 ikifuatiwa na Soko la hisa DSE ikiwa na 
asilimia 36 na ya tatu ni Benki ya NMB yenye asilimia 9.
Taarifa hiyo iliendelea kueleza 
kuwa ukubwa wa mtaji wa soko umeshuka kwa asilimia 0.03 na kufikia 
shilingi trilioni 22.7 kutoka trilioni 23.4 wiki iliyopita na ukubwa wa 
mtaji wa makampuni ya ndani umeshuka kwa 0.01% na kufika Trilioni 8.3 
kutoka trilioni 8.4 wiki iliyopita
Mbali na hayo taarifa hiyo 
imeeleza kwamba licha ya mauzo kushuka lakini pia viashiria vya soko 
katika sekta ya viwanda vimeshuka kwa alama imeshuka kwa alama 66.10 
baada ya bei za hisa za TBL kushuka kwa 2.13% pamoja na kaunta za  DSE 
kwa asilimia  na DCB kwa asilimia 14.
Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa 
viashiria vya soko katika sekta ya huduma za kibiashara wiki hii imebaki
 kwenye hali yake ya wiki iliyopita baada ya bei za hisa za Swissport 
kubaki shilingi  3,543.02.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni