Alhamisi, 25 Agosti 2016

Bodi Mpya Yaanza Kazi Rasmi Muhimbili


MBI1
Msimamizi wa Chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), Trustworthy Majuta akieleza mafanikio na changamoto kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Charles Majinge (wa tatu kulia) na wajumbe wa bodi hiyo. Kutoka kulia ni Mtaalamu wa Mapafu kwa wagonjwa waliozidiwa, Dk Alex Masau, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Charles na Msimamizi wa Jengo la Mwaisela, Adelini Jacob.
MBI2
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Charles Majinge, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Charles (mwenye koti) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru wakiwa katika chumba cha CT-Scan ambako wagonjwa wanachukuliwa vipimo.
MBI3
Mkuu wa Kitengo cha Ufuaji, Linah Kinabo akiwaeleza wajumbe wapya wa bodi ya Muhimbili jinsi wanavyofanya kazi na changamoto mbalimbali katika kitengo hicho.
MBI4
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru (kulia), Mwenyekiti mpya wa Bodi, Profesa Charles Majinge na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Grace Magembe wakiendelea na ziara katika hospitali hiyo.  
MBI5
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, Koo na Sikio, Dk Edwin Liyombo akiwaeleza jambo wajumbe wa bodi hiyo walipoetembelea hospitali hiyo.
MBI7
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Hospitali hiyo, Makwaia Makani (kushoto) na  Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Charles wakiingia kwenye wodi za wagonjwa wenye matatizo ya afya ya akili.
MBI8
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharula na Ajali katika Hospitali ya Muhimbili, Dk Juma Mfinanga akiwaeleza wajumbe wa bodi  kazi zinazofanywa na idara hiyo.
MBI10
Sehemu ya Jengo la Idara ya Magonjwa ya Dharula na Ajali likiwa limekarabatiwa kwa ajili ya kutoa huduma bora na kisasa kwa wagonjwa mbalimbali. (Picha na John Steven MNH)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni