Bodi Mpya Yaanza Kazi Rasmi Muhimbili
Msimamizi wa Chumba cha wagonjwa 
wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), Trustworthy Majuta akieleza 
mafanikio na changamoto kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya
 Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Charles Majinge (wa tatu kulia) na 
wajumbe wa bodi hiyo. Kutoka kulia ni Mtaalamu wa Mapafu kwa wagonjwa 
waliozidiwa, Dk Alex Masau, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, 
Isaya Charles na Msimamizi wa Jengo la Mwaisela, Adelini Jacob.
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa 
Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Charles
 Majinge, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Charles (mwenye 
koti) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence 
Museru wakiwa katika chumba cha CT-Scan ambako wagonjwa wanachukuliwa 
vipimo.
Mkuu wa Kitengo cha Ufuaji, Linah 
Kinabo akiwaeleza wajumbe wapya wa bodi ya Muhimbili jinsi wanavyofanya 
kazi na changamoto mbalimbali katika kitengo hicho.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa 
Muhimbili, Profesa Lawrence Museru (kulia), Mwenyekiti mpya wa Bodi, 
Profesa Charles Majinge na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk 
Grace Magembe wakiendelea na ziara katika hospitali hiyo.  
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, 
Koo na Sikio, Dk Edwin Liyombo akiwaeleza jambo wajumbe wa bodi hiyo 
walipoetembelea hospitali hiyo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa 
Hospitali hiyo, Makwaia Makani (kushoto) na  Mstahiki Meya wa Jiji la 
Dar es Salaam, Isaya Charles wakiingia kwenye wodi za wagonjwa wenye 
matatizo ya afya ya akili.
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya 
Dharula na Ajali katika Hospitali ya Muhimbili, Dk Juma Mfinanga 
akiwaeleza wajumbe wa bodi  kazi zinazofanywa na idara hiyo.
Sehemu ya Jengo la Idara ya 
Magonjwa ya Dharula na Ajali likiwa limekarabatiwa kwa ajili ya kutoa 
huduma bora na kisasa kwa wagonjwa mbalimbali. (Picha na John Steven 
MNH)
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni