WAZIRI SIMBACHAWENE SERIKALI ITATEKELZA AHADI ZAKE.
Na Sheila Simba,MAELEZO
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais 
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene amesema kuwa 
 Rais Magufuli amedhamiria kuwatumikia wananchi na kuhakikisha maendeleo
 yapatikani kwa Watanzania wote.
Akizungumza katika kipindi kipya
 cha “TUNATEKELEZA” kinachoandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO na TBC1 
Waziri Simbachawene alisema kuwa serikali ipo kwa ajili ya kufanya kazi 
ya kuwatumikia wananchi katika kila sekta ili kutatua changamoto 
zinazowakabili.
“Kupitia falsafa yetu ya hapa 
kazi tu tutahakikisha tunawaletea wananchi maendeleo kutokana na ahadi 
zilizoaidiwa kutoka katika ilani 2015-2020 ya Chama Cha Mapinduzi 
kilicho na serikali.”
Alisisitiza kuwa Rais Magufuli 
ameamua kuleta mabadiliko ya kweli hapa nchini ambayo yanalenga kuwabana
 wabadhirifu wa mali za umma na kurejesha kurejesha nidhamu ya kazini 
jambo ambalo limeanza kuonekana katika Ofisi mbalimbali za umma.
Waziri huyo amewahakikishia 
wananchi  kuwa ahadi za maendeleo zilizotolewa na Serikali ya awamu ya 
tano zitatekelezwa kama ilivyopangwa kwani wanayo dhamira ya kweli ya 
kuwatumikia wananchi.
Alisema kuwa suala la 
kusimamiana kazini ni la kawaida na ni wajibu wa kila mtumishi hakikishe
 anatimiza wajibu wake katika nafasi aliyopewa ili aweze kutekeleza 
majukumu yake kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wa serikali kwa 
kuweka uzalendo mbele.
Aliongeza kuwa ari na nidhamu ya
 utendaji kazi mikoani imebadilika na watu wanafanya kazi kuhakikisha 
wananchi wanapata huduma bora,kwani baadhi ya watumishi wa Halmashauri 
walikuwa wanafanya kazi kwa mazoea.
Kuhusu watumishi hewa alisema 
kuwa serikali imeondoa watumishi 12,000 waliokua wananchukua mishahara 
bila kufanya kazi na kuomba wananchi kuunga mkono juhudi za serikali 
katika hatua wanazochukua.
“upangaji mzuri wa watumishi 
kwenye maeneo ya utoaji huduma kwa wananchi kwa maana ya Halmashauri 
utakuwa umekaa vizuri kwa asalimia kubwa hata kwa kuwapanga vizuri bila 
wafanyakazi hewa kuwepo”alifafanua Waziri Simbachawene 
Alisema kuwa suala la wataalamu 
wa fani mbalimbali kupendelea kubaki mijini ni tabia na kukosa uzalendo 
kwani baadhi ya watumishi wanaopagiwa mikoani hawaripoti kutokana na 
mazingira jambo ambalo sio sahihi.
“hata huku mijini wanakokimbilia
 hakuna nyumba za watumishi basi imekuwa ni tabia tu ya watu kukosa 
uzalendo”alisema Simbachawene.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni