WANAFUNZI WA CHUO CHA DIPLOMASIA WAMNUNULIA MWENZAO VIFAA VYA KUMSAIDIA KUSIKIA, ANA UWEZO MKUBWA DARASANI PAMOJA NA MATATIZO YAKE
Kaimu Mkuu wa Chuo Cha Diplomasia 
Dk Bernald Achiula akizungumza na waandishi wa habari chuoni hapo wakati
 akishukuru wanafunzi wa chuo hicho kwa michango yao waliyochanga ili 
kumsaidia mwanafuzni mwenzao Shinuna Salum Nyamkokwa ambaye ana matatizo
 ya kusikia, wanafunzi hao wamechanga Fedha na kumnunulia mwenzao Vifaa 
vya kumsaidia kusikia vyenye thamani ya shilingi milioni moja na laki 
tano,  Kulia ni Mwanafuzni  Shinuna Salum Nyamkokwa  ambaye ameelezewa 
kuwa ana uwezo mkubwa katika masomo yake darasani pamoja na kutokuwa na 
uwezo wa kusikia,  na Katikati ni Neema Zawadi Henjewele Makamu wa Rais 
Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia.
Neema Zawadi Henjewele Makamu wa 
Rais Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia akielezea kwa 
waandishi wa habari kuwa kitu kilichowafanya  wanafunzi  wa chuo hicho 
kumchangia mwanafunzi mwenzao Shinuna Salum Kulia  ni kutokana na uwezo 
wake katika masomo pamoja kuwa tatizo la usikivu linalomkabili
Mwanafuzni huyo Shinuna Salum 
Nyamkokwa akizungumza mbele ya waandishi wa habari wakati akielezea 
kuhusu msaada wa vifaa hivyo ambapo amesema awali kichwa kilikuwa 
kinamuuma sana lakini kwa sasa hakiumi tena.
Gordian Kilave Mkuu wa Idara ya 
Lugha Chuo cha Diplomasia akielezea matatizo yaliyokuwa yakimkuba na 
kumsumbua mwanafunzi Shinuna Salum kabla ya kupatiwa vifaa hivyo ambavyo
 ninamsaidia kusikia kwa sasa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni