NSSF yamuunga mkono Rais Magufuli, yatoa mkopo wa bil 4/- kwa kiwanda cha viuadudu Kibaha.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la 
Taifa la Hifadhi ya jamii (NSSF)Prof Godius Kahyarara (kulia) akikabidhi
 mfano wa hundi ya pesa yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 2 na
 laki 1 (zaidi ya Tsh bilioni nne) kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la 
Taifa la Maendeleo (NDC)  Dkt Samuel Nyantahe (wa tatu kushoto) ikiwa ni
 mkopo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji kwenye kiwanda  cha kuzalisha  
viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu cha Tanzania Biotech Product  Ltd 
kilichopo wilayani Kibaha, mkoani Pwani wakati wa hafla fupi ya 
makabidhiano iliyofanyika mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni pamoja na 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye 
Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (katikati), Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Bi 
Assumpta Mshana, (wa pili kulia) Mkurugenzi wa huduma za sheria wa Benki
 ya Azania, Bw Geofrey Dimoso (wa pili kushoto) na Kaimu Meneja Mkuu wa 
kiwanda hicho Bw Samwel Mziray.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama 
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Bi Assumpta Mshana pamoja na  jopo la maofisa 
 kutoka NSSF, NDC, benki ya Azania na uongozi wa kiwanda cha kuzalisha  
viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu cha Tanzania Biotech Product kwa 
pamoja wakimsiliza mmoja wa wataalam kutoka kiwanda hicho aliekuwa 
akifafanua moja ya shughuli za kiwanda hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama 
(kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya
 jamii (NSSF)Prof Godius Kahyarara (kushoto) pamoja na viongozi wa NSSF 
kwenye ziara hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama 
(kulia) akimpongeza mmoja wa wataalamu wazalendo waliopo kwenye kiwanda 
hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama 
pamoja na jopo la viongozi kutoka NSSF, NDC, benki ya Azania na uongozi 
wa kiwanda cha kuzalisha  viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu cha 
Tanzania Biotech Product kwa pamoja wakimsiliza Kaimu Meneja Mkuu wa 
kiwanda hicho Bw Samwel Mzirayaliekuwa akifafanua uwezo wa viuadudu 
vinavyozalishwa na kiwanda hicho.
………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu,
SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya 
Jamii (NSSF) limetoa mkopo wa dola za kimarekani  mil. 2.1 (zaidi ya sh 
bilioni nne) kwa kiwanda  cha kuzalisha  viuadudu vya kuua viluwiluwi 
vya mbu cha Tanzania Biotech Product  Ltd kilichopo wilayani Kibaha, 
mkoani Pwani ili kukiongezea uzalishaji wake, hatua inayotajwa kuwa ni 
kuitikia wito wa Rais Dr John Magufuli wa kuifanyaTanzania kuwa nchi ya 
viwanda.
Mbali na mkopo huo unaotolewa 
kupitia benki ya Azania itayayosimamia urejeshwaji wake, pia shirika 
hilo lipo kwenye mchakato wa kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vipya na 
vikubwa zaidi vya kutengezeza nguo, matairi pamoja na sukari hapa 
nchini.
Akizungumza wilayani Kibaha 
mwishoni mwa wiki wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mkopo huo kwa 
Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) linalomiliki kiwanda hicho, 
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara alisema shirika lake lina
 dhamira ya dhati katika kuwekeza kwenye viwanda nchini ili kuongeza 
fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Tanzania.
“Pamoja na kuitikia wito wa Rais 
Dr John Magufuli katika kuibadilisha Tanzania kuwa nchi ya viwanda ili 
kuiongeza ajira hapa nchini lakini pia tunatarajia kupata faida kupitia 
marejesho ya pesa hizi,’’ Alibainisha.
Akiwatoa hofu wanachama wa mfuko 
huo na watanzania kwa ujumla kuhusu usalama wa pesa zao, Prof Kahyarara 
alisema uamuzi wa shirika kuwekeza kwenye viwanda sio mgeni kwa kuwa 
ulianza miaka ya nyuma ambapo shirika hilo liliwezesha viwanda vya 
saruji Mbeya, Mkonge Tanga, Sukari Kagera na kiwanda cha nguo 21st Century cha Morogoro.
“Uwekezaji huo ulionyesha 
mafanikio makubwa kwa wananchi wengi walipata ajira na shirika lilipata 
faida iliyokusudiwa na kuboresha mafao ya wananchama.  Tupo makini na 
aina za uwekezaji na miongoni mwa kanuni tunazotumia katika uwezaji ni 
suala la tija, faida, usalama na malengo ya mradi husika hususani katika
 kuinua uchumi wa nchi kwa ujumla,’’ alisema.
Akizungumza kwenye hafla 
hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu 
wenye Ulemavu) Mhe, Bi Jenista Mhagama mbali na kulipongeza shirika hilo
 kwa kuunga mkono nia ya Rais na serikali kwa ujumla katika kuelekea 
uchumi wa viwanda, alisema uwezeshaji wa kiwanda hicho  umeongeza kasi 
ya vita dhidi ya ugonjwa wa Malaria kwa asilimia tisini (90).
“Kiwanda hiki ni cha kipekee 
barani Afrika na ufanisi wake utawanufaisha si tu watanzania bali 
Waafrika kwa ujumla na kutuletea fedha za kigeni,’’ alisema.
Alisema uamuzi wa shirika hilo 
kutoa mkopo huo kupitia benki ya Azania utaliwezesha shirika hilo kuwa 
na msimamizi thabiti wa marejesho ya pesa za wanachama wa mfuko huo.
“Mwanzo kabisa kwenye uamuzi huu  
niliomba kupata uhakika fedha za wanachama na nilipohakikishiwa kuwa 
kuna benki itasimamia mkopo huu basi nikajua pesa za wanachama zipo 
salama. Niendelee tena kuwaomba wahusika wote wawe makini kwenye pesa 
hizi,’’ alisisitiza.
Alitoa wito kwa mifuko ya hifadhi 
hapa nchini kuhakikisha inawekeza zaidi kwenye viwanda huku akiwataka 
viongozi wa mashirika mbalimbali kuhakikisha wanalinda haki na maslahi 
ya wafanyakazi wao likiwemo suala la kuwaunganisha wafanyakazi wao na 
 mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi
 ya NDC Dkt Samuel Nyantahe alisema mkopo huo utakiwezesha kiwanda hicho
 ambacho kimejengwa kwa kushirikiana na kampuni ya LABIOFAM SA ya nchini
 Cuba kupanua uzalishaji wake na kuwa katika nafasi ya kutafuta soko 
hadi nje ya nchi.
Naye Mkurugenzi wa huduma za 
sheria wa Benki ya Azania, Bw Geofrey Dimoso alisema benki yake 
imejipanga kuhakikisha inasimamia urejeshwaji wa pesa hizo kwa mfuko wa 
NSSF huku akiwatoa hofu wanachama wa mfuko huo kuwa pesa zao zipo 
salama.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni