Jumatano, 31 Agosti 2016

Baraza la ushauri latoa zawadi kwa wanafunzi walioshinda kwenye insha


TOL1
Kaimu katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  anayesimamia sekta Mawasiliano mhandisi Dkt. Maria Sasabo kushoto akizungumza wakati wa hafla ya kutoa zawadi kwa wanafunzi wa vyuo, sekondari na shule za msingi za jijini Dar es Salaam walioshinda shindano la uandishi wa insha kuhusu haki ya mtumiaji wa huduma za mawasiliano, kulia ni Katibu wa Baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za mawasiliano  Bi. Mary Shao Msuya.
TOL2
Mwenyekiti wa baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za mawasiliano Bw. Stanley Mwabulambo akimkaribisha mgeni rasmi  Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  (Mawasiliano) Mhandisi Dkt. Maria Sasabo kuzungumza na wanafunzi wa vyuo, sekondari na shule za msingi za jijini Dar es Salaam walioshinda shindano la uandishi wa insha kuhusu haki ya mtumiaji wa huduma za mawasiliano  
TOL3
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa vyuo vya elimu ya juu Bw. Omari Abbas kutoka chuo Kikuu kishiriki cha Ualimu (DUCE) akipokea zawadi ya cheti kutoka kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  (Mawasiliano) mhandisi Dkt.   Maria Sasabo.
TOL4
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa Shule za sekondari Bw, Ramadhani Mohamed kutoka Shule ya sekondari ya Kibasila  akipokea zawadi ya mshindi wa kwanza wa insha kutoka kwa Kaimu katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  (Mawasiliano) mhandisi Dkt. Maria Sasabo.
TOL5
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa Shule za Msingi  Jane Michael Andrew  kutoka shule ya msingi ya Mbuyuni akipokea zawadi ya cheti ya mshindi wa kwanza wa insha kutoka kwa Kaimu katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  (Mawasiliano) mhandisi Dkt. Maria Sasabo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni