Alhamisi, 11 Agosti 2016

NETBALL TANZANIA YAANZA VYEMA MASHGINDANO YA MAJESHI


net1
Mchezaji Nasra  Suleiman wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 (Picha na Selemani Semunyu)
net2
Mchezaji  Faraja Malaki wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 (Picha na Selemani Semunyu)
net3
Mchezaji  Veronica Patrick wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 (Picha na Selemani Semunyu)
net4
Mchezaji  Veronica Patrick wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 (Picha na Selemani Semunyu)
……………………………………………………………………………………………….
Na Selemani Semunyu JWTZ
Timu ya Mpira wa Pete Netball ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ime3rejesha heshima yake baada ya Kuwafunga mabingwa Watezi  wa Michuano hiyo kwa Mpira wa Pete Uganda kwa magoli 29 kwa 27.
Katika Mchezo huo uliokuwa wa Vuta nikuvute  na rabsha za hapa na pale zilizizojitokeza kabla wakati na Baada ya Mchezo huo ambao ulikuwa na Upinzani Mkali kutokana na historia ya Timu hizo.
Katika Robo ya Kwanza Tanzania ilimaliza ikiongoza kwa magoli saba kwa Sita huku Timu zote zikicheza Mchezo wa kuviziana lakini uliojaa nguvu na kukamiana miongoni mwa Wachezaji.
Katika Robo ya Pili Tanzania pia ilimalizai ikiwa mbele kwa mabao 13 kwa 11 kukiwa na tofauti ya magoli mawili tofauti na robo ya kwanza ambayo ilimalizika kwa tofauti ya goli moja.
Robo ya Tatu Uganda walikuja na kusawazisha na kasha kuongeza na hivyo kumaliza kwa ushindi wa magoli 20 kwa 19 ya Tanzania  na kuwafanya Tanzania kwenda kujiuliza.
Hatimaye robo ya Mwisho ikamalizika na Timu ya Tanzania kuibuka na Ushindi na hivyo kuwatisha Mabingwa wa mwaka uliopita pengine utarejea kwa Tanzania
 Kwa Upande wa Nahodha wa Timu hiyo Dorita Mbunda alisema mechi yao na Uganda wamecheza kama fainali kutoka na historian a kuahidi kujipanga kwa ajili ya kuwakabili Kenya. 
Kwa upande wake Nahodha Uganda Lilian Ajio amelalalimika Waamuzi kutoelewa Sheria Mpya za Mchezo huo hali iliyopelekea wakati mwingine kutokuwa na maamuzi sahihi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni