MKUTANO WA LOWASSA NA WANAFUNZI MUHIMBILI WAZUILIWA
Na Dotto Mwaibale
……………………..
UONGOZI
 wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Shirikishi Muhimbili (MUHAS) umezuia 
mkutano uliokuwa ufanywe na baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho na Waziri 
Mkuu wa zamani Edward Lowaasa.
Mkutano
 huo ambao ulikuwa ufanyike na baadhi ya vijana wa kikristo ambao ni 
wanafunzi wa chuo hicho ulikuwa pangwa kufanyika juzi chuoni hapo 
kuanzia saa za mchana.
Akizungumza mtandao wa www. habari za jamii.com 
 mmoja wa wanafunzi hao ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema 
maandalizi yote ya mkutano huo ambao ulikuwa baada ya ibada yalikuwa 
yamekamilika.
“Tulifanya
 taratibu zote ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo 
ambao ulitukubalia na kumualika ndugu Lowassa lakini tumeshangazwa na 
zuio lililotolewa na uongozi wa chuo” alisema mwanafunzi huyo.
Mwanafunzi
 huyo alisema kuwa saa sita mchana wakati wakimsubiri mgeni rasmi Edward
 Lowassa awasili mkuu wa chuo hicho na viongozi wengine waliwaita na 
kuwaeleza kwamba mkutano huo umewekewa zuio kutoka juu hivyo 
hautafanyika bila ya kutoa sababu .
Msemaji
 wa Lowassa Abubakar Lihongo alisema wanafunzi hao baada ya kuzuiliwa 
kufanya mkutano huo walimuomba radhi Lowassa na kumueleza watamualika 
tena kipindi kingine wakiwa tayari.
“Mimi
 naona zuio hilo linatokana na masuala ya kisiasa lakini kuna barua ya 
wanafunzi hao ipo katika mitandao ya kijamii mkiipata mnaweza kupata 
picha halisi” alisema Liongo.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni