MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWASILI MJINI MBABANE SWAZILAND TAYARI KWA MKUTANO WA 36 WA SADC
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu 
Hassan akiwasili kwenye ardhi ya mji wa Mbabane nchini Swaziland tayari 
kuhudhuria mkutano wa 36 wa SADC wa Wakuu wa nchi  na Serikali ambao 
utafanyika tarehe 29 Agosti mjini hapo.
 Sehemu ya Mabinti wa Swaziland wakiimba na kucheza wakati wa mapokezi ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
akipokelewa na ngoma mbali mbali mjini Mbabane nchini Swaziland.
 Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
(kushoto) akizungumza na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. 
Phiwayinkhosi Mabuza wa Swaziland ambaye pia ni Kaimu Waziri wa Fedha 
mara baada ya kuwasili kwenye kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mfalme
 Mswati III.
………………………………………………………
………………………………………………………
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan 
amewasili mjini Mbabane – Swaziland leo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano 
wa 36 wa Wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa 
Afrika- SADC.  
Makamu
 wa Rais Samia Suluhu Hassan atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano 
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano huo ambao utafanyika 
tarehe 29 Agosti  2016 ambapo Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa nafasi ya
 Uenyekiti wa Jumuiya hiyo.
Mkutano
 huo wa 36 wa SADC ni maalum kwa wakuu wa nchi na serikali wanaounda 
Kamati ya siasa,ulinzi na usalama ambao watajadili kwa kina hali ya 
siasa na usalama, demokrasia na maombi ya Burundi na Comoro kwa ajili ya
 kujiunga na SADC.
Makamu
 wa Rais Samia Suluhu Hassan katika  msafara wake amefuatana na Waziri 
wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa 
Augustine Mahiga, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles 
Mwijage na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya 
Mapinduzi ya Zanzibar Amina Salum Ali.
 



 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni