MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI, MHE. GEORGE MASAJU AVIASA VYAMA VYA SIASA KUHESHIMU KATIBA YA NCHI
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mh.
 George Masaju akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam 
wakati alipoelezea masuala mbalimbali ya  kisheria yanayozuia 
maandamano  ya Ukuta yaliyoitishwa na Chama cha Demokrasia na Mendeleo 
CHADEMA, kulia ni Asiatu Msuya Ofisa habari wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu
 wa Serikali.
………………………………………………………………………………..
Na Hassan Silayo
MAELEZO -Dar es Salaam.
VYAMA vya siasa nchini 
vimetakiwa kutumia vyema haki zao za msingi zilizoanishwa katika katiba 
badala ya kutumia nguvu ubabe na kupelekea kutishia hali ya amani ana 
utulivu iliyopo nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini 
Dar es Salaam na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju wakati wa 
mkutano wake na Wahariri wa vyombo vya habari akizungumzia kuhusu wajibu
 wa utii wa sheria na kudumisha amani nchini.
Mhe. Masaju alisema kumekuwa na 
baadhi ya wanasiasa wanaotoa vitisho vya kuitisha mikutano kinyume na 
taratibu za kisheria kwa kisingizio cha haki za kikatiba jambo ambalo 
sio kweli.
“Napenda kuvishauri vyama vya 
siasa nchini kuacha kutumia kauli za kibabe na vitisho kwa kisingizio 
cha kutumia haki zao za kikatiba, hali hiyo itapelekea vyombo vya dola 
 kuchukua hatua kwani ni viashiria vya uvunjifu wa amani”.
Masaju aliwataka Wanasiasa kuwa 
wakweli na kuacha kuwapotosha wananchi kuwa wananyimwa haki ya kufanya 
mikutano kwani wapo baadhi yao wanaofanya mikutano katika majimbo yao 
baada ya Jeshi la Polisi kujidhirisha kwamba kutakuwa na hali ya amani 
na utulivu”. Alisema Mhe. Masaju.
Aidha Masaju alipongeza juhudi 
zinazofanywa na viongozi mbalimbali wa dini nchini kwa jitihada 
wanazofanya za kushauri katika kufika muafaka wa hali ya kisiasa nchini 
na kuwashauri kuhubiri amani na utulivu kwa waumini wao.
Akitoa ufafanuzi wa tamko la 
baadhi ya vyama vya upinzani kutaka serikali kuvifuta vyama hivyo Mhe. 
Masaju alisema kuwa suala hilo ni kinyume na katiba ya Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania kwa sababu katiba hiyo inaruhusu mfumo wa vyama 
vingi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni