Ijumaa, 26 Agosti 2016

SERIKALI YA MKOA WA IRINGA YAPONGEZA TUZO YA UBORA WA MAZIWA KUTOKA KAMPUNI YA ASAS DAIRIES LTD


AS1
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas Dairies Ltd  baada ya kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa Afrika  tuzo ya ARSO leo wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  pichani  kutoka kushoto  wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  Roy Omulo ,mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri  na mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela kulia
AS2
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela ( mwenye suti katikati) akiwasili  eneo la  warsha  kwa ajili ya ufungaji  kushoto  kwake ni mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd Ahmed Abri na  washiriki  wengine
AS3
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kufungua maziwa kabla ya kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas Dairies Ltd  baada ya kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa Afrika  tuzo ya ARSO wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  pichani  kutoka kushoto  wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  Roy Omulo ,mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri  na mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela kulia
AS4
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (katikati)ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akifunga warsha ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kwa  wafugaji 35 kutoka mkoa wa Iringa , Mbeya na Njombe leo ,kushoto wa kwanza ni meneja biashara na maendeleo  wa kampuni ya maziwa  ya Asas akifuatiwa na mkurugenzi wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri na kulia  ni mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela
………………………………………………………………….
Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI  ya  mkoa  wa  Iringa  imeipongeza kampuni ya  maziwa ya Asas Dairies Ltd ya  mkoani Iringa  kwa kushinda tuzo  ya (ARSO) kwenye  mashindano ya  kimaifa ya nchi  za Africa ya  ubora  wa bidhaa za maziwa  kuwa ni tuzo yenye heshima kubwa kwa mkoa huo na Tanzania kwa ujumla .
Pamoja na pongezi hizo  pia imepongeza  jitihada  zinazofanywa na kampuni ya  Asas Dairies  Ltd  kwa  kuwawezesha mafunzo  mbali mbali wafugaji  wa mikoa ya Mbeya , Njombe na  Iringa  kubadili  ufugaji wa  kienyeji na  kufuga  kibiashara  zaidi  .
Huku  ikiwataka wenye  viwanda  vya  usindikaji  maziwa kujenga utamaduni  wa  kuwafikia  wafugaji na  kuwapa   elimu  ili  kuwezesha  bidhaa zao  za maziwa  kuendelea   kuwa  zenye  ubora  zaidi  na  ikiwezekana  kuwawezesha  kupata vifaa vya  kisasa  vya  kukamulia maziwa.
Kaimu  mkuu  wa  mkoa wa Iringa Richard Kasesela  aliyasema hayo leo  kwenye ukumbi wa Asas mjini hapa  wakati wa  ufungaji wa mafunzo ya wiki moja kwa wafugaji 35  kutoka Iringa , Mbeya  na Njombe  mafunzo yaliyoandaliwa kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT  CTF
Alisema kuwa kampuni  hiyo  imeupa mkoa wa Iringa  heshima  kubwa na kuwa ukiacha mashindano mbali mbali ya maziwa kwa viwanda  vya ndani ya  Tanzania kampuni  hiyo imekwisha  shinda mara nne  sasa jambo ambalo ni la kujipongeza na kujivunia kuwa bidhaa  zinazozalishwa ni bora na hivyo si wakati wa watanzania  kukimbilia bidhaa za nje na kuacha zinazozalishwa ndani ya nchi .
Kasesela ambae  pia ni mkuu wa wilaya  ya Iringa  alisema kuwa mbali ya  wadau na wawekezaji  waliopo katika wilaya  yake na mkoa wa Iringa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni