SERIKALI YA MKOA WA IRINGA YAPONGEZA TUZO YA UBORA WA MAZIWA KUTOKA KAMPUNI YA ASAS DAIRIES LTD
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa 
Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa 
akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  
yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na 
kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT
 kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas Dairies Ltd  baada ya 
kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa Afrika  tuzo ya ARSO leo 
wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  pichani  kutoka kushoto  
wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  Roy Omulo ,mkurugenzi 
mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri  na mwakilishi wa  
katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela kulia 
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa 
Richard  Kasesela ( mwenye suti katikati) akiwasili  eneo la  warsha  
kwa ajili ya ufungaji  kushoto  kwake ni mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd 
Ahmed Abri na  washiriki  wengine
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa 
Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa 
akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  
yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na 
kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT
 kufungua maziwa kabla ya kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas
 Dairies Ltd  baada ya kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa 
Afrika  tuzo ya ARSO wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  
pichani  kutoka kushoto  wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  
Roy Omulo ,mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed 
Abri  na mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John 
Mosela kulia
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa 
Richard  Kasesela (katikati)ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akifunga 
warsha ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la 
umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  
wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kwa  wafugaji 35 kutoka mkoa 
wa Iringa , Mbeya na Njombe leo ,kushoto wa kwanza ni meneja biashara na
 maendeleo  wa kampuni ya maziwa  ya Asas akifuatiwa na mkurugenzi wa 
kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri na kulia  ni mwakilishi wa  
katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela
………………………………………………………………….
Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI  ya  mkoa  
wa  Iringa  imeipongeza kampuni ya  maziwa ya Asas Dairies Ltd ya  
mkoani Iringa  kwa kushinda tuzo  ya (ARSO) kwenye  mashindano ya  
kimaifa ya nchi  za Africa ya  ubora  wa bidhaa za maziwa  kuwa ni tuzo 
yenye heshima kubwa kwa mkoa huo na Tanzania kwa ujumla .
Pamoja na pongezi hizo  pia 
imepongeza  jitihada  zinazofanywa na kampuni ya  Asas Dairies  Ltd  
kwa  kuwawezesha mafunzo  mbali mbali wafugaji  wa mikoa ya Mbeya , 
Njombe na  Iringa  kubadili  ufugaji wa  kienyeji na  kufuga  
kibiashara  zaidi  .
Huku  ikiwataka wenye  viwanda  
vya  usindikaji  maziwa kujenga utamaduni  wa  kuwafikia  wafugaji na  
kuwapa   elimu  ili  kuwezesha  bidhaa zao  za maziwa  kuendelea   kuwa 
 zenye  ubora  zaidi  na  ikiwezekana  kuwawezesha  kupata vifaa vya  
kisasa  vya  kukamulia maziwa.
Kaimu  mkuu  wa  mkoa wa Iringa 
Richard Kasesela  aliyasema hayo leo  kwenye ukumbi wa Asas mjini hapa 
 wakati wa  ufungaji wa mafunzo ya wiki moja kwa wafugaji 35  kutoka 
Iringa , Mbeya  na Njombe  mafunzo yaliyoandaliwa kilimo  biashara  
yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na 
kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  
SAGCOT  CTF
Alisema kuwa kampuni  hiyo  
imeupa mkoa wa Iringa  heshima  kubwa na kuwa ukiacha mashindano mbali 
mbali ya maziwa kwa viwanda  vya ndani ya  Tanzania kampuni  hiyo 
imekwisha  shinda mara nne  sasa jambo ambalo ni la kujipongeza na 
kujivunia kuwa bidhaa  zinazozalishwa ni bora na hivyo si wakati wa 
watanzania  kukimbilia bidhaa za nje na kuacha zinazozalishwa ndani ya 
nchi .
Kasesela ambae  pia ni mkuu wa 
wilaya  ya Iringa  alisema kuwa mbali ya  wadau na wawekezaji  waliopo 
katika wilaya  yake na mkoa wa Iringa
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni