NBS yapokea msaada wa Bil. 25 kwa ajili ya watoto
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango 
Mhe. Ashatu Kijaji akionyesha Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa 
Tanzania mbele ya wadau mbalimbali wa takwimu hawapo pichani wakati wa 
uzinduzi wa taarifa hiyo jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango 
Mhe. Ashatu Kijaji akiongea mbele ya wadau mbalimbali wa takwimu hawapo 
pichani wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa 
Tanzania jijini Dar es salaam.
Wadau mbalimbali wa takwimu 
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji hayupo
 pichani wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa 
Tanzania jijini Dar es salaam.
……………………………………………………………………………………
Na Ally Daud-Maelezo
Tume ya Taifa ya Twakimu (NBS) 
imepokea msaada wa shilingi bilioni 25 kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili 
ya kusaidia kuboresha tasnia ya takwimu kuhusu haki za watoto nchini.
Akizungumza kwenye hafla ya 
uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa Tanzania Naibu 
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji amesema kuwa amepokea 
msaada huo kwa nia ya kuendeleza tasnia ya takwimu nchini na kusaidia 
malengo ya nchi ya miaka mitano.
“Tumepokea msaada huu kwa furaha 
na hamasa kubwa katika kufikia lengo letu la kuboresha na kukuza tasnia 
ya takwimu nchini ili kuweza kupata taarifa muhimu kwa ajili ya 
maendeleo ya miaka mitano ya nchi yetu”. Alisema Mhe. Kijaji.
Aidha Mhe. Kijaji amesema kuwa 
Wizara yake imewapa kipaumbele watoto kwa kutenga shilingi. Bilioni 18 
kila mwezi ili kuwasaidia katika mambo  muhimu ya kila siku hususani 
elimu bora, makazi na malazi.
Mbali na hayo Mhe. Kijaji 
ameshukuru na kuwapongeza Umoja wa ulaya kwa msaada huo na kuwataka 
wasichoke kuwa nao pamoja katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu 
ya mwaka 2030.
Kwa upande wa Mwakilishi wa Balozi
 wa Umoja wa Ulaya Bw. Eric Beaume  Amesema kuwa msaada huo sio mwisho 
wao kwani wanapenda kazi ya NBS na matokeo yake hivyo wapo tayari kutoa 
kiasi kikubwa zaidi ili kuwezesha tume hiyo kutoa takwimu zenye uhakika 
kwa maendeleo ya Tanzania.
Bw.Beaume amesema kuwa Umoja wao 
utakua bega kwa bega na Tanzania katika kutoa misaada ili kusaidia haki 
zote za watoto ili kujenga taifa lenye tija na muamko wa kimaendeleo 
kutokana na takwimu zitokanazo na tume hiyo.
Aidha Bw. Beaume ameongeza kuwa 
Umoja wao upo tayari kusaidia Nyanja za kilimo, Nishati katika maeneo ya
 vijijini ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika kufikia
 malengo ya maendeleo endelevu kwa miaka mitano ijayo.
Mbali na hayo Mkurugenzi Mkuu wa 
NBS Dkt. Albina Chuwa amesema  kutokana na msaada huo wamepata hamasa 
kubwa kwa tume hiyo kuweza kupambana na kupata takwimu yakinifu 
zitazopelekea kuleta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali yahusuyo jamii 
nchini na kufikia malengo ya miaka mitano.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni