POLISI KUBORESHA VITUO VYAKE VYA AFYA.
Naibu Inspekta Jenerali wa 
Polisi, Abdulrahman Kaniki akizungumza na Washiriki wa Mkutano wa 
kutathmini mradi wa kupambana na ukimwi na kifua kikuu unaotekelezwa na 
Jeshi la Polisi katika vituo vyake vya Afya kumi na tano hapa nchini 
 kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la JSI-AIDS Free tawi la 
Tanzania.Mkutano huo wa siku tatu unafanyika mkoani Dodoma.Kulia ni 
Mganga mkuu wa Polisi Dk.Janda Lushina na Kamanda wa Polisi Mkoa wa 
Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Lazaro Mambosasa 
(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)  Baadhi
 ya Maofisa wa Polisi ambao ni Washiriki wa Mkutano wa kutathmini mradi 
wa kupambana na ukimwi na kifua kikuu ndani ya Jeshi la Polisi 
wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano huo mkoani Dodoma.Mradi 
huo unaotekelezwa na Jeshi la Polisi katika vituo vyake vya Afya kumi na
 tano hapa nchini  kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la 
JSI-AIDS Free tawi la Tanzania. (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi
……………………………………………………………………………………………………………….
Baadhi
 ya Maofisa wa Polisi ambao ni Washiriki wa Mkutano wa kutathmini mradi 
wa kupambana na ukimwi na kifua kikuu ndani ya Jeshi la Polisi 
wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano huo mkoani Dodoma.Mradi 
huo unaotekelezwa na Jeshi la Polisi katika vituo vyake vya Afya kumi na
 tano hapa nchini  kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la 
JSI-AIDS Free tawi la Tanzania. (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi
……………………………………………………………………………………………………………….
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Dodoma
Jeshi la Polisi nchini 
litaendelea kuboresha vituo vyake vya afya ili kuwawezesha Askari kupata
 huduma zilizo bora jambo ambalo litawawezesha kufanya kazi wakiwa na 
afya pamoja na morali katika kupambana na uhalifu nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu 
Inspekta Jenerali wa Polisi, Abdulrahman Kaniki Mkoani Dodoma wakati wa 
ufunguzi wa Mkutano wa  kutathmini mradi wa kupambana na ukimwi na kifua
 kikuu unaotekelezwa na Jeshi la Polisi katika vituo vyake vya Afya kumi
 na tano hapa nchini  kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la 
JSI-AIDS Free tawi la Tanzania.
Kaniki alizitaja juhudi 
zinazoendelea kuchukuliwa kuwa ni pamoja na kuboresha majengo, kutoa 
mafunzo kwa watendaji pamoja na kuhakikisha kuwa hospitali za Polisi 
zinakuwa na vifaa bora kwa mujibu wa viwango vilivyowekwa na Wizara ya 
Afya .
Aidha alitoa wito kwa Shirika 
la JSI-AIDS Free kuongeza wigo wa huduma zake katika vituo vngine 
ambavyo havijafikiwa na mradi huo hapa nchini ili kuhakikisha kuwa kila 
mahali palipo na kituo cha Afya cha Polisi kunakuwepo na mradi huo ambao
 umesaidia sana askari na watumiaji wengine wa huduma hizo.
Kwa upande wake Mwakilishi 
mkazi wa Shirika hilo kwa upande wa Tanzania Dk.Beati Mboya alisema 
lengo la mkutano huo ni kufanya tathmini ili kubaini mafanikio na 
changamoto zinazovikabili vituo vinavyotekeleza mradi huo ilikuzipatia 
ufumbuzi.
Alisema wanatarajia kufanya 
tathmini hiyo kila baada ya miezi mitatu ili kuhakikisha hakuna 
ucheleweshaji katika kutoa huduma baada ya kubaini changamoto na 
kuzifanyia kazi kwa haraka.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Afya
 cha Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Paul 
Kasabago alisema kikosi hicho kitaendelea kutoa huduma zilizobora ili 
kuimarisha afya za Askari na familia zao kote nchini licha ya kukabiliwa
 na upungufu wa wahudumu wa Afya.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni