WAZIRI PROF.MBARAWA ATOA MIEZI MIWILI KUKAMILISHA UJENZI WA barabara ya Mangaka-Nakapanya
 Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akisalimia 
na wananchi wa Tunduru, baada ya kukagua barabara ya Tunduru-Nakapanya 
KM 66.5, Mkoani Ruvuma.
………………………………………………………………………………………..
Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ametoa miezi 
miwili kwa mkandarasi wa kampuni ya M/s Jiangxi Geo-Engineering (Group) 
Corporation anayejenga sehemu ya barabara ya Mangaka-Nakapanya yenye 
urefu wa Km 70.5 kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha 
lami.
Amesema
 hayo wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Tunduru-Mangaka-Mtambaswala 
inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km 202.5 ambayo 
kukamilika kwakwe kutafungua fursa za kiuchumi na kuunganisha mikoa ya 
Ruvuma, Mtwara na Lindi.
Amebainisha
 kuwa Mpango wa Serikali ni kuwajengea watanzania miundombili bora 
itakayowafikisha katika uchumi wa kati ifikapo 2025 hivyo haitamvumilia 
Mkandarasi anayechelewesha kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali 
inayotekelezwa hapa nchini.
“Natoa
 miezi miwili mkandarasi uwe umemaliza hii barabara, wananchi wa Mangaka
 na Tanzania kwa ujumla wanahitaji kuanza kuitumia kwa ajili ya kuinua 
uchumi wa Taifa”, amesema Waziri Prof. Mbarawa.
Waziri
 Mbarawa ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa fedha kwa Makandarasi 
wanaotekeleza miradi mbalimbali nchini hivyo lazima wajipange kumaliza 
kazi kwa wakati na kuzingatia viwango vya ubora kulingana na makubaliano
 ya  mkataba.
Aidha
 amesisitiza kuwa Serikali haitaingia mkataba mwingine kwa mkandarasi 
yoyote ambaye hatakamilisha kazi kwa wakati kulingana na makubaliano.
Kwa 
upande wake Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) mkoa wa
 Mtwara Eng. Dotto John amemhakikishia Waziri Mbarawa kusimamia mradi 
huo ili ukamilike kwa wakati na kuchochea maendeleleo ya Mikoa ya 
kusini.
“Wananchi
 wamengojea kwa muda mrefu kukamilika kwa mradi huu ili uwe kichocheo 
cha maendeleo hivyo  ninakuhakikishia kuwa nitawasimamia kwa umakini 
makandarasi ili wazingatie vigezo tulivyokubaliana kwenye mkataba”, 
amesisitiza Eng. Dotto.
Waziri
 Prof. Mbarawa amekagua mradi wa ujenzi wa barabara ya 
Tunduru-Mangaka-Mtambaswala yenye urefu wa km 202.5 inayojengwa kwa 
kiwango cha lami ambapo kukamilika kwake kutafungua fursa za kiuchumi 
mikoa ya Kusini ikiwemo kuiunganisha Tanzania na Msumbiji kwa lami 
kupitia daraja la umoja lililoko Mtambaswala.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni