“NAVY KENZO KUMSINDIKIZA MISS TANGA 2016”
 NA, MWANDISHI WETU TANGA
MSANII
 wa Mziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania Navy Kenzo anatarajiwa 
kutumbuiza kwenye shindano la kumtafuta malkia wa Mkoa wa Tanga Miss 
Tanga 2016 litakalofanyika Julai 29 mwaka huu kwenye ukumbi wa Hotel ya 
Tanga Beach Resort.
Licha
 ya Navy Kenzo wasanii wengine ambao watasindikiza onyesho hilo kwa 
kutoa burudani ni kundi la mziki wa kizazi kipya mkoani Tanga,Wazenji 
Classic pamoja na Dances.
Akizungumza
 jana,Mratibu wa Onyesho hilo, alisema kuwa maandalizi ya kuelekea 
shindano hilo yanaendelea vizuri ambapo tayari warembo watakaoshiriki 
wameanza kuingia kambini .
Shindano
 hilo ambalo limeandaliwa na kituo cha Radio cha TK FM 88.5 kilichopo 
mjini Tanga kwa kushirikiana na Hotel ya Tanga Beach Resort wameelezea 
namna walivyo jipanga kuhakikisha onyesho hilo linakuwa na ushindani 
mkubwa kutokana na aina ya warembo waliopo .
 
 “Nisema tu tumejiandaa vizuri kuhakikisha shindano hilo linafanyika kwa
 umakini mkubwa ili kuwawezesha wadau wa tasnia ya urembo mkoani hapa 
kuweza kupata ladha halisi ya onyesho hilo kwani licha ya kuwaona 
warembo wakali wakini pia mzee wa kamatia chini atakuwepo kuwapagawisha
“Alisema.
“Alisema.
Hata
 hivyo alisema kuwa mazoezi ya warembo watanaoshiriki onyesho hilo 
yanaendelea kwenye ukumbi wa New Hotel uliopo mjini hapa kuanzia saa 
kumi jioni.
Aidha
 alisema kuwa kabla ya kufanyika shindano hilo warembo hao watapata 
fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii mkoani hapa 
ikiwemo Mapango ya Amboni na Hifadhi ya Taifa ya Saadani.
Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
 

 
KING CASINO, LLC GIVES A $100 FREE BET
JibuFutaKING CASINO, LLC GIVES A $100 FREE jancasino.com BET https://jancasino.com/review/merit-casino/ to try. Visit us today and receive 출장안마 a $100 FREE BET! Sign herzamanindir.com/ up at our new https://octcasino.com/ site!