KALA JEREMIAH, SUPER NYAMWELA KUPAMBA MSIMU MPYA WA JUKWAA LA SANAA LA BASATA
Msimu
 mpya wa Jukwaa la Sanaa unatazamiwa kuzinduliwa rasmi Jumatatu ya 
tarehe 25/07/2015 kwenye Ukumbi wa BASATA ulioko Ilala Sharif Shamba 
jijini Dar es Salaam kuanzia saa saa 4:00 Asubuhi – 6:30 Mchana.
Wasanii
 hawa wanatarajiwa kuupamba uzinduzi huo kwa kutoa burudani mbalimbali 
sambamba na kuongea na wasanii wachanga katika kuwahamasisha na 
kuwajengea uwezo juu ya namna wanaweza kutumia fursa mbalimbali za 
mashindano ya kukuza vipaji katika kujijenga kisanaa.
BASATA
 linatambua kwamba kumekuwa na tatizo la wasanii katika kutambua na 
kuchangamkia fursa mbalimbali zilizoko katika sekta ya Sanaa hasa zile 
zilizomo kwenye mashindano mbalimbali ya kutafuta vipaji ambayo wasanii 
Kala Jeremiah na Super Nyamwela wamekuwa wakishiriki kikamilifu.
Ushiriki
 wa wasanii hawa katika kuwajengea hamasa na kuwapa changamoto wasanii 
wachanga utasadia katika kuwajengea uwezo wa kutumia fursa hizo.
Mbali
 na burudani na elimu hiyo, uzinduzi huu wa msimu wa mpya wa Jukwaa la 
Sanaa unaotarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya mia moja (100) 
utahusisha pia kongamano maalum ambalo litajikita katika kutoa elimu 
mbalimbali kuhusu sekta ya Sanaa kwa wadau watakaohudhuria.
Jukwaa
 la Sanaa ni programu iliyobuniwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) 
kwa lengo la kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo sekta ya 
Sanaa lakini pia kusaidia waandishi wa habari kupata habari zihusuzo 
sekta ya Sanaa kutoka vyanzo mahsusi.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
Imetolewa na Kitengo cha Habari
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni