Msemaji kutoka kituo cha Sibuka Televisheni wa kwanza kulia Bw.
George Nangale akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati
wa uzinduzi wa kipindi cha INABAMBA “Ni bongo movie bandika bandua”
kitachokuwa kinaonyeshwa katika kituo hiko cha matangazo uliofanyika leo
jijini Dar es salaam, kushoto ni Afisa habari wa kampuni ya Step
Entertainment Bw. Moses Mwanyilu.
Mkurugenzi wa matamasha kutoka kampuni ya usambazaji filamu nchini Steps Entertainment katikati
Bw. Jonas Sabuni akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati
wa uzinduzi wa kipindi cha INABAMBA “Ni bongo movie bandika bandua”
ambao uliofanyika leo jijini Dar es salaam, kushoto ni Afisa habari wa
kampuni hiyo Bw. Moses Mwanyilu na kulia ni mwigizaji wa bongo movie
Jimmy Mafufu.
Afisa
habari wa kampuni ya Step Entertainment Bw. Moses Mwanyilu wa kwanza
kushoto akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa
uzinduzi wa kipindi cha INABAMBA “Ni bongo movie bandika bandua”
kitachokuwa kinaonyeshwa katika kituo cha matangazo Sibuka Televisheni
uliofanyika leo jijini Dar es salaam,katikati ni , Msemaji kutoka kituo
cha Sibuka Televisheni Bw. George Nangale na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Masoko kutoka Startimes Bw. Awino Felia.
Meneja
Masoko kutoka Startimes Bw. Awino Felia wa kwanza kushoto akiongea na
waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa kipindi cha
INABAMBA “Ni bongo movie bandika bandua” kitachokuwa kinaonyeshwa katika
kituo cha matangazo Sibuka Televisheni kupitia king’amuzi cha
Startimes uliofanyika leo jijini Dar es salaam
PICHA ZOTE NA ALLY DAUD-MAELEZO.
………………………………………………………….
Na Beatrice Lyimo MAELEZO Dar es Salaam
WASANII
wa Filamu nchini wanatarajia kunufaika na kazi zao kufutia makubiliano
ya Kampuni ya Star Media Tanzania Ltd (Startimes), pamoja na Steps
Entertainment za kutumia kazi zao kwenye vituo vya televisheni nchini.
Akizungumza
waandishi wa habari leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Sibuka Media, Dkt.
George Nangale alisema kazi hiyo itafanywa kwa ushirikiano na taasisi
hizo ili kuweza kuwasaidia wasanii kunufaika na kazi zao kupitia luninga
badala ya kuwasubiri wateja wao kuzinunua katika santuri (DvD).
“Tumefikia
uamuzi huu baada ya kuona ombwe lililopo sasa katika kuzifikisha filamu
zetu kwa walio wengi pamoja na kwamba Watanzania wana mwamko mkubwa wa
kuzitazama filamu hizi zenye mafunzo ya maisha na burudani” alisisitiza
Mkurugenzi huyo.
Kwa
upande wake Msanii wa Bongo Movie, Mwanaheri Hamad alisema uonyeshaji
wa kazi zao katika vituo vya televisheni utawanufaisha wasanii chipukizi
ambao kazi zao bado hazijaonekana.
Amesema
kuwa kutokana na mkataba huo wa kurusha filamu hzo umerahisisha soko za
kazi hizo katika mfumo DvD ambapo ulikuwa unatumiwa hapo awali.
Filamu
hizo zitaonyeshwa kupitia king’amuzi cha StarTimes chaneli 111
ikijulikana kama Sibuka Maisha Steps chaneli kila siku na itaanza
kuonyeshwa Ijumaa hii tarehe 29 Julai, 2016.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni