KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO
WAKATI
 wasanii wa kundi la ngoma za utamaduni la Utandawazi wanajipanga 
kutumbuiza, watu wengi waliokusanyika kwenye viwanja wa shule ya msingi 
Bukongo mjini Nansio walikuwa wanajiuliza mtoto Gozbert Bwele (8) 
aliyekuwa amekumbatia ngoma alikwenda kufanya nini pale.
Lakini
 mara tu ngoma zilipoanza kupigwa, uwanja mzima ukalipuka kwa furaha na 
haikushangaza wakati makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria 
Teresa Fernandez de la Vega, aliposhindwa kuvumilia na kutoka kwenda 
kucheza na mtoto huyo aliyeonyesha
ufundi mkubwa katika upigaji wa ngoma. Mama Maria Teresa, ambaye ni rais wa taasisi ya Mfuko wa kusaidia Wanawake Afrika, alijitoma uwanjani kucheza na kumtunza mtoto huyo anayesoma darasa la kwanza kwenye shule ya msingi Nansole katika halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza.
ufundi mkubwa katika upigaji wa ngoma. Mama Maria Teresa, ambaye ni rais wa taasisi ya Mfuko wa kusaidia Wanawake Afrika, alijitoma uwanjani kucheza na kumtunza mtoto huyo anayesoma darasa la kwanza kwenye shule ya msingi Nansole katika halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza.
Makamu
 huyo wa Rais mstaafu wa Hispania alizuru kisiwani Ukerewe akiwa 
ameongozana na ujumbe wake kwa lengo la kujionea kilimo cha viazi lishe 
na usindikaji wa mazao mbalimbali yatokanayo na viazi hivyo. Kilimo 
hicho kinafanywa na akinamama 25 chini ya Mradi wa Green Voices 
unaofadhiliwa na taasisi ya Mfuko wa kusaidia Wanawake Afrika, ambao kwa
 hapa nchini  umewawezesha wanawake wa Tanzania kubuni miradi endelevu 
inayoendana na utunzaji wa mazingira pamoja na kupambana na mabadiliko 
ya tabianchi
 



 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni