MAN UTD DORTMUND KUFUNGUA PAZIA LA MICHUANO YA ICC ITAKAYOONEKANA KUPITIA STARTIMES
  Na Dotto Mwaibale
 IKIWA
 chini ya kocha wake mpya Mreno, Jose Mourinho, Manchester United 
wanatarajia kushuka dimbani jijini Shanghai, China kuwakabili Borrusia 
Dortmund siku ya Ijumaa Julai 22, 2016 mechi itakayopigwa saa tisa za 
alasiri kwa saa za hapa nyumbani kupitia ving’amuzi vya StarTimes.
Akizungumzia
 juu ya habari hiyo njema kwa wapenda soka nchini Makamu wa Rais wa 
StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amebainisha kuwa michuano hiyo 
itakuwa ni ya kusisimua kutokana na orodha ndefu ya timu kubwa 
zitakazoshiriki kama vile Real Madrid, Barcelona, Manchester United, 
Manchester City, Paris Saint-Germain, Juventus, Liverpool, Chelsea na 
Bayern Munich kwa uchache.
“Tunayofuraha
 kuwatangazia wateja wetu na watanzania kwa ujumla kuwa watapata fursa 
ya kutazama timu zao katika mechi za awali kabla ya kuanza kwa ligi kuu 
mbalimbali duniani kupitia ving’amuzi vya StarTimes pekee. Mechi zote za
 michuano ya ICC itaonekana moja kwa moja kupitia chaneli ya World 
Football inayopatikana katika kifurushi cha Mambo kwa malipo ya shilingi
 12000/- tu kwa mwezi. Michezo yote itakuwa ni yenye msisimko mkubwa 
kwani timu zinazoshiriki ni kubwa, nyingi zikiwa ni mabingwa katika ligi
 kuu zao, zina wachezaji nyota na kikubwa zaidi zingine hazikuwahi 
kukutana kabla.” Alisema Bi. Hanif
“Hii
 ni fursa ya pekee kwa watanzania kwani tunafahamu ya kuwa ni wapenzi 
wakubwa wa mchezo huu na siku zote StarTimes tunajitahidi kuwapatia kile
 wanachokipenda. Hii ni mara ya pili tunaonyesha moja kwa moja michuano 
hii kwani mwaka jana tulifanya hivyo ambapo timu ya Real Madrid 
waliibuka mabingwa. Hivyo basi mashabiki watakuwa na shauku kubwa ya 
kujua ni timu gani itakayoibuka mabingwa au kama utarudi kwa Real 
Madrid,” alisema na kumalizia Bi. Hanif kuwa, “Ni wajibu wetu 
kuhakikisha wanafikiwa na matangazo ya vipindi vizuri na kusisimua kama 
hivi kwa ubora wa hali ya juu na gharama nafuu ambazo kila mtu 
atazimudu.”
Mchezo
 huo ni sehemu ya ufunguzi wa michuano ya kombe la mabingwa wa kimataifa
 almaarufu kama International Champions Cup au ICC itakayoanza kutimua 
vumbi Julai 22 na kumalizika Agosti 13, 2016 katika viwanja mbalimbali 
nchini Marekani, Ulaya, Australia na China.
Katika
 michuano hii wapenzi wa soka duniani watapat fursa kujionea kwa mara 
kwanza mechi ya watani wa jadi kutoka jiji la Manchester au 
unavyojulikana kama ‘Machester Derby’ miongoni mwa mashabiki wengi. 
Mechi hiyo itapigwa siku ya Jumatatu ya Julai 25 jijini Beijing, China.
Mchezo
 huo utanogeshwa si tu na ushindani baina ya wachezaji au mashabiki bali
 safari hii ni makocha waliopewa vibarua vya kunoa vikosi hivyo, Jose 
Mourinho wa Manchester United na Pep Guardiola wa Manchester City.
Ukiachana
 na mechi hiyo, pia macho ya mashabiki wengi yatakuwa yakisubiria kwa 
hamu kutazama mechi kali zitakazozikutanisha timu za, Real Madrid na 
 PSG,  Chelsea na Liverpool, Real Madrid na Chelsea, Bayern Munich na 
Real Madrid pamoja na Liverpool na Barcelona.
Kwa
 ujumla timu zitazoshiriki  michuano hii ni pamoja na Real Madrid, 
Barcelona, Manchester United, Manchester City, Paris Saint-Germain 
(PSG), Juventus, Liverpool, Chelsea, Bayern Munich, Liverpool, Tottenham
 Hotspurs, AC Millan, Inter Millan, Leicester City FC, Celtic FC, 
Atletico Madrid, Melbourne Victoria na South China.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni