JB, Mataluma, Kitime ndani ya igizo ya kuhamasisha Kilimo
………………………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu
Msanii
nyota nchini wa filamu, Jacob ‘JB’ Steven ni miongoni mwa waigizaji
mbalimbali walioshiriki katika igizo la Kumekucha ambayo imeandaliwa
kwa ajili ya kuhamasisha vijana kujishughulisha na kilimo kutokana na
uhaba wa soko la ajira.
Igizo
hilo ambali pia ni mchezo wa redio (radio plays) limeandaliwa na
taasisi ya Africa Lead kwa kushirikiana na Media For Development
International (MFDI) chini ya udhamini wa Shirika la Kimataifa la
Maendeleo (Usaid) ya ushauri wa Taasisi ya chakula na lishe (TFNC),
Taasisi ya TAHA, ACDI VOCA – NAFAKA, Land O Lakes, Rudi, Mwanzo Bora,
The Rice Council of Tanzania, Technoserve, ANSAF (Non State Action
Forum) na taasisi ya AMSHA.
Katika
filamu hiyo, JB anatumia jina la Mzee Kidevu ambaye kazi yake kubwa ni
kununua mazao kwa wakulima kwa bei ya ukandamizaji na kuwafanya wakulima
hao kuendelea kuwa na maisha duni huku yeye akijinufaisha.
Akizungumza
katika uzinduzi huo, JB alisema kuwa amefurahi sana kushiriki katika
filamu hiyo ambayo inafundisha na kuhamasisha vijana kujihusisha zaidi
na masuala ya kilimo na kuacha tabia ya kukimbilia mijini kama suluhisho
lao la kutatua matatizo yao.
“Nimepanda
kushiriki katika filamu na mchezo huu wa redio, umenipa mwanga mkubwa
na kupanua wigo wa kazi yangu ya kuigiza, kabla ya kuingia kwenye
kuigiza, nilikuwa mnunuzi wa mazao hasa mahindi kule Kibaigwa na kusaga
na kuuza unga wa chakula, hii ilikuwa fursa kwangu na nimeipenda,
nawashukuru wahusika wote waliofanikisha filamu hii,” alisema JB.
Mkurugenzi
wa masuala ya Uchumi wa USAID, Randy Chester alisema kuwa wamefurahi
kujihusisha na masuala mbalimbali yaa maendeleo hapa nchini na kuamua
kusaidia mradi huo ambao unahusika zaidi maeneo ya vijini.
“USAID
imejihusisha katika miradi mingi ya maendeleo nchini, kama unajua,
zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania wanajihusisha na masuala ya kilimo,
waahitaji kuendelezwa ili kufikia hatua kubwa ya maendeleo, mchezo wa
Kumekucha utawaamsha na kupata maendeleo,” alisema Chester.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni