TAARIFA YA UTEUZI WA VIONGOZI KATIKA TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dkt. ALI Mohamed Shein amefanya uteuzi wa viongozi katika Taasisi mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa
na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Dkt.
Abdulhamid Y. Mzee, katika Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dkt. Juma Yakout Juma ametuliwa kuwa Naibu Katibu Msaidizi
Baraza la Mapinduzi (Sera, Ufuatiliaji na Tathmini).
Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Sera na Utafiti ameteuliwa Nd. Mwadini Makame Haji.
Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria,
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mkurugenzi wa Mipango, Sera na Utafiti
Nd. Abdalla Issa Mgongo na Mkurugenzi wa Miundo ya Taasisi, Utumishi na
Maslahi ya Watumishi Nd. Shaibu Ally Mwazema.
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa,
Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa Nd. Khalid Omar Abdalla na Katibu wa Tawala wa
Wilaya ya Magharibi ‘A’ Nd. Mashaka Hassan Mwita.
Katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais Nd. Issa Mlingoti Ally ameteuliwa kuwa Mratibu Mkuu wa Ofisi ya
Uratibu wa Shughuli za SMZ, Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Sera na Utafiti Nd. AMEIR Makame Ussi
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa
shughuli za Serikali Nd. Khalid Bakari Amran, Mkurugenzi wa Idara ya
sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa Nd. Riziki Daniel Yussuf na Ofisa
Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba Nd. Ali Salim Alim
Matta.
Wizara ya Afya Mkurugenzi wa
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti Nd. Ramadhan Khamis Juma na Ofisa
Mdhamini wa Wizara ya Afya Pemba Nd. Ali Bakari Ali.
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na UvuviMkurugenzi wa Umwagiliaji Maji Nd. Haji Hamid Saleh.
Wizara ya Habari, Utalii,
Utamaduni na Michezo Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa na Sensa ya
Filamu na Utamaduni Dkt. Omar Abdalla Adam.
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na
Usafirishaji Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Nd. Abdalla A.
Mwinyigogo na Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo Nd. Ramadhan Mussa Bakari.
Katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Omar Ali Omar Bhai ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi.
Wizara ya Ardhi, Mji, Nishati na
Mazingira Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Nd. Tahir M. K. Abdalla na
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Maji na Nishati
(ZURA) Nd. Hemed Salim Hemed.
WIZARA YA Biashara Viwanda na Masoko Mkurugenzi wa Mipango, sera na Utafiti Nd. Nana Mwanjisi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni