Jumapili, 17 Julai 2016

NAIBU WAZIRI WAMBURA ASIKILIZA CHANGAMOTO ZA MCHEZO WA RIADHA KUTOKA KWA JOHN AKHWARI MWANARIADHA MKONGWE

ste1Mwanariadha wa zamani aliyewahi kushika nafasi ya pili duniani katika mashindao ya     Olimpiki nchini Ugiriki  Bw. John Stephen Akhwari  (wa kwanza kulia) akimuonyesha Naibu Waziri wa Habari Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura (katikati) Mwenge aliyoukimbiza katika viwanjani vya Beijing nchini China wakati wa kufungua mashindano ya Olimpiki mwaka 2008 alipomtembelea nyumbani kwake katika Kijiji cha Khaday, Kata ya Sanu Mjini Mbulu,(wakwanza kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Bw.Chelestino Mofuga.
ste2Naibu Waziri wa Habari Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura (katikati) akiwa ameshikilia kikombe cha ushindi wa Mwanariadha wa zamani John Stephen Akhwari alichoshinda shinda katika Mashindano yaya Olimpiki yaliyofanyika nchini Ugiriki kwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Bw.Chelestino Mofuga (wa kwanza kushoto)  na  John Steven Akhwari mwenye (wa kwanza kulia) wakiwa nyumbani kwake katika Kijiji cha Khaday, Kata ya Sanu.
ste4Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akisalimiana na Daktari wa Timu ya Jeshi la Wananchi Andrew Panga leo alipotembelea timu hiyo kambini Mjini Mbulu  akiwa katika ziara ya kikazi (wakwanza kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Bw.Chelestino Mofuga.
ste3Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura(wasita kulia) akiwa katika picha ya pamoja leo na Timu ya wanariadha wa Jeshi la Wananchi waliyoko kambini Wilayani Mbulu alipowatembelea akiwa katika ziara ya kikazi (wasita kushoto) ni mwanariadha wa zamani John Stephen Akhwari pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Bw.Chelestino Mofuga.
akw1Mwanariadha wa zamani aliyeweka rekodi ya Kimataifa ya kuonyesha Uzalendo kwa nchi  yake katika mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Mexico mwaka 1968  kwa  kuendelea kukimbia na kushika namba mbili  mbali na kwamba alikuwa amevunjika mguu  wakati  akiwa uwanjani Bw.John Stephen Akhwari  akileza changamoto za sekta ya riadha nchini katika Mkutano wa wadau wa kisekta na Naibu Waziri Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura (hayupo pichani) ulifofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara.
akw2Mwanariadha wa zamani aliyeiletea Tanzania sifa kwa kushinda mashindano mbalimbali ya Kimataifa na kupata Medali za aina mbalimbali Bw.Alfredo Shahanga  akieleza changamoto zilizojitokeza wakati wadau wa kutoka nchini Australia walipokuja Tanzania na kutaka kujenga uwanja wa michezo Wilayani Mbulu kumuenzi mwanariadha mzalendo John Stephen Akhwari kwa Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura (hayupo pichani) leo katika mkutano wa wadau wa kisekta Mkoani Manyara.
Na Anitha Jonas- MAELEZO,BABATI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni