PROF. MBARAWA AFUNGUA MKUTANO WA NNE WA WADAU WA SIMU
………………………………………………………………………………………….
Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amezungumzia 
umuhimu wa wananchi wa mjini na vijijini kutumia simu ili waweze 
kunufaika na huduma mbalimbali za kimtandao zinazotumika hapa nchini.
Akizungumza
 mara baada ya kufungua mkutano wa nne wa kimataifa wa chama cha kampuni
 za simu duniani GSMA mobile 360, Prof . Mbarawa amesema Serikali 
imejipanga kuhakikisha miundombinu ya mawasiliano ya simu inawafikia 
wananchi wote ili kuwezesha kunufaika na huduma za simu za kisasa.
‘Ili 
wananchi waweze kupata maendeleo kwa haraka  na kunufaika na fursa za 
kimtandao katika masuala ya elimu, biashara, kilimo, afya na ustawi wa 
jamii kwa ujumla kunahitajika uwepo wa simu za kisasa zinazoweza 
kuruhusu mifumo ya kimawasiliano’, Amesema Waziri Prof. Mbarawa.
Ameitaja
 mifumo hiyo kuwa ni Elimu Mtandao, Afya Mtandao, Biashara Mtandao,  
Kilimo Mtandao, Serikali Mtandao, Hali ya Hewa Mtandao ambavyo kwa 
pamoja  vitamhudumia mwananchi kwa ubora na wakati.
Amesisitiza
 kuwa serikali inashirikiana kwa karibu na kampuni  za mawasiliano ya 
simu ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha huduma za simu zinakuwa za 
uhakika na salama.
Serikali
 inaendelea kuhakikisha kwamba mfuko wa Mawasiliano Vijijini unaendelea 
kunufaisha watanzania na mkakati wa kuhakikisha umeme unafika vijijini 
unaimarika sambamba na uwepo wa simu za kisasa za bei nafuu.
Takribani laini za simu milioni 39.9 nchini zinatumika katika huduma mbalimbali na hivyo huchangia uchumi wa nchi.
Waziri
 Prof. Mbarawa amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kuweka mazingira 
mazuri ya uwekezaji ili kukuza sekta ya mawasiliano hapa nchini ambapo 
hadi sasa tayari kilomita 18,000/- za mkongo wa taifa wa taifa wa 
mawasiliano zimejengwa hapa nchini.
“Serikali
 itaendelea kudhibiti vifaa vya mawasiliano visivyo na ubora ili 
visiingie nchini na hivyo kuhakikisha watumiaji wa mitandao ya simu 
wanakuwa salama na wanaitumia mitandao hiyo kwa wakati wote’. 
Amesisitiza Prof. Mbarawa.
Mkutano
 huo wa siku mbili ambao pia umehudhuriwa na Naibu Waziri Mkuu wa Nchi 
ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Bw. Thomas Luhaka ambapo 
pamoja na mambo mengine utajadili Changamoto mbalimbali na kuja na 
suluhisho na namna bora ya kuendeleza Sekta ya Mawasiliano duniani.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni