TBL Group yadhamini semina ya wakaguzi wa magari wa polisi Mwanza
………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu-Mwanza
Katika
 mkakati wake wa  kushirikiana na serikali na jamii katika kutoa elimu 
ya usalama,kampuni ya TBL Group imedhamini semina kwa  wakaguzi wa 
magari kutoka Jeshi la Polisi jijini Mwanza ambayo imefanyika katika 
kiwanda cha TBL cha Mwanza na kuendeshwa na Mtaalamu wa magari kutoka 
kampuni ya CFAO,Bw.Hubert Kubo.
Semina
 hiyo iliendeshwa kwa  njia shirikishi ambapo  washiriki walijadiliana 
masuala mbalimbali yanayohusiana na usalama barabarani na changamoto 
zilizopo katika kukagua vyombo vya moto na  jinsi ya kupunguza ajali za 
barabarani nchini.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni