SERIKALI YATOA MSIMAMO WAKE KUHUSU BENKI YA TWIGA BANCORP
 Msajili
 wa Hazina, Lawrence Mafuru (katikati), akizungumza katika mkutano na 
waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu msimamo wa Serikali kuhusu
 Benki ya Twiga Bancorp. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, 
Cosmas Kimario na Mkurugenzi  Rasilimali Watu na Utawala, Amina Lumuli.
 Maofisa wa Benki hiyo wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Mpiga picha za magazeti Loveness Benard akiwa kazini ‘ hapana kuchezea kazi hapa kazi tu’
……………………………………………………………………
MSAJILI
 wa Hazina Ndugu Lawrence Mafuru ametolea ufafanuzi taarifa iliyotolewa 
na vyombo vya habari kuhusu msimamo wa Serikali kwa Benki ya 
Twigabancorp.
Taarifa
 hiyo ilieleweka vibaya kuhusu msimamo wa Serikali kwa benki hii ya 
Twiga Bancorp. Naomba nieleze kwamba kwa hivi sasa Serikali inasubiri 
mapendekezo ya kitaalamu yatakayowezesha kutatua changamoto za kimtaji 
za Twiga Bancorp. 
Ninaposema
 changamoto za kimtaji sijasema kwamba benki hiyi ipo kwenye hali mbaya 
ya kushindwa kujiendesha, ila inahitaji nyongeza ya mtaji kwa ajili ya 
kutekeleza matakwa ya kisheria na vilevile kuimarisha na kusambaza 
huduma mbalimbali katika maeneo ya nchi. Hatua hizo zinafuatia agizo la 
Mheshimiwa Rais kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipangokufuatilia 
utendaji wa benki ya Twiga Bancorp na kuhakikisha kasoro zilizopo 
zinatatuliwa.
“Kuna
 njia mbalilimbali za kuiwezesha benki kupata mtaji ikiwemo nje ya 
utaratibu wa Serikali, ndiyo maanaWizara na Ofisi ya Msajili wa Hazina 
ikishirikiana na Manejiment ya Twiga Bancorp zinaandaa mapendekezo 
yatakayoiwezesha Benki hii kupata mtaji ili kuiwezeshakutimiza malengo 
yake ya kiukuaji na kujiendesha kwa faida.”
Hatua
 mbalimbali zilianza kuchukuliwa na Wizara ya Fedhana Mipango na ofisi 
ya Msajili wa Hazina kwa ajili ya kuboresha utendaji wa Benki ya Twiga 
Bancorp. Kwa mfano, mnamo mwaka 2015, Muundo wa Shirika ulibadilishwa 
ambao pamoja na mambo mengine ulipelekea kuteuliwa kwa Menejimenti mpya,
 kwa kupitia Menejimenti hiyo mpya  umetengenezwa Mpango Mkakati wa 
miaka mitano ambao umeanza kutumika Januari 2016, serikali pia ilifanya 
mabadiliko katika bodi ya wakurugenzi kwa kuteuaBodi mpya ya 
Wakurugenzi. 
Kwa
 ujumla kuna mabadiliko makubwa ya kiutendaji baada ya hatua hizo 
kuchukuliwa. Kwa mfano benki imeweza kupata Hati Safi ya Mahesabu 
(Unqualified Opinion) kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Heasabu za 
Serikali kwa mara ya kwanza kwenye hesabu zake za mwaka 2015 jambo 
ambalo halikuwezekana toka Mwaka 2011. 
“Hizi
 taarifa zinazosambaa kuwa benki inafungwa sio za kweli. Kwenye benki 
kuna pesa za wananchi, kuna mikopo iliyotolewa kwa watu mbalimbali, kuna
 rasilimali za benki ikiwemo rasilimmali watu. Yote hayo yana Utaratibu 
wake wa kuyasimamia.. Hata ukisikiliza hotuba ya Rais hakusema funga 
benki ya Twiga Bancorp aliagiza hatua zichukuliwe na kwamba Katibu Mkuu 
asimamie.” 
Hivyo
 tuna wahakikishia kuwa fedha za wananchi zilizo katika benki ya Twiga 
Bancorp zipo salama na kwamba uongozi uliopo hivi sasa unaendelea 
kushughulikia changamoto za kiutendaji zilizokuwepo na kama yalivyokuwa 
maagizo ya Rais hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa kwa ajili ya 
kuhakikisha mambo yote yanakuwa sawa. Pia benki hii inaendelea kutoa 
huduma zake kwa wateja kama kawaida.”
Mwisho,
 Serikali itaendelea kutoa msukumo kwa benki hiiili kuhakikisha tatizo 
lililopo sasa la mtaji linatatuliwa na kuhakikisha inajiendesha kwa 
faida. 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni