BFA YAPATA VIONGOZI WAPYA WA MIAKA MINNE IJAYO
………………………………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
CHAMA
 cha mpira wa miguu ,wilayani Bagamoyo,mkoa wa Pwani,( BFA) kimechagua 
viongozi wapya wa chama hicho wataokingoza katika kipindi cha miaka 
minne .
Uchaguzi huo umefanyika kihalali ,kwa mujibu wa sheria ambao ulihudhuliwa na wajumbe 91.
Katika
 uchaguzi huo alhaj AbdulZahoro Sharifu alichaguliwa kuwa mwenyekiti kwa
 kipindi kitakachoishia mwaka 2020 kwa kupata kura 77.
Alhaj
 Sharif alipata ushindi huo kwa kupata kura hizo dhidi ya mpinzani wake 
Kitomu Yona aliyepata kura 11 huku nafasi ya makamu mwenyekiti 
alichaguliwa Shaabani Makelele ambae hakuwa na mpinzani.
Nafasi
 ya katibu mkuu imenyakuliwa na John Fransis Bolizozo “Boli Kubwa” 
aliyejipatia kura 81 na kumwacha mbali mgombea mwenzie kwenye nafasi 
hiyo Yona Mkawa aliyejinyakulia  kura 4.
Katibu
 msaidizi alishinda Jitihada Omary kwa kura zote kutokana na kuwa peke 
yake ,mhazini alichaguliwa Ornjurie Marigwa ambae hakuwa na mpinzani 
 msaidizi ikienda kwa Salumu Kanuti aliyejikusanyia kura 88.
Mjumbe
 mkutano mkuu wa mkoa alichaguliwa kipa wa zamani wa nyota nyekundu na 
kocha mzawa hapa nchini Shekhe Abdallah aliyepata kura 45 dhidi ya kura 
43 alizopata Mzee Minjoli.
Nafasi
 ya mwakilishi wa vilabu akichaguliwa Jabir Omary aliyeshinda kwa kura 
46 akimwacha mgombea mwenzake Ally Jakaya aliyepata kura 44.
Wajumbe
 kamati ya utendaji na kura zao katika mabano waliochaguliwa ni 
Ramadhani Mape (77), Rajabu Maliki (80), Maneno Kidobe (68), Shabani 
Masimbi (69) na Peter Nyambasi (39).
Katika
 uchaguzi huo uliongozwa na mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wilaya 
Mwinyi Akida, mwenyekiti aliyemaliza muda wake Shaabani Kangale 
“Machokodo” na diwani wa kata ya Kiwangwa Hussein Malota Kwaga.
Baada
 ya kutangaza matokeo hayo Akida aliwataka viongozi hao kuhakikisha 
wanawatumikia ipasavyo wana-Bagamoyo ili mpira uchezwe maeneo yote.
Alieleza
 kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kukidhi kiu ya wana michezo ambao kwa 
muda mrefu hususan ukanda wa Chalinze na maeneo mengine wilayani humo 
ambao wamekosa fursa hiyo.
Nae
 mwenyekiti mpya wa BFA ,Abdul Sharif, alitoa rai kwa viongozi wengine 
wa chama hicho kuhakikisha kila mmoja anajitoa kwa hali na mali ili 
kuinua sekta ya michezo wilayani humo.
Alhaj
 Sharif aliahidi kupatikana kwa timu itakayocheza ligi kuu ya Vodacom 
Tanzania Bara katika kipindi cha miaka minne ambacho watakiongoza.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni