Jumapili, 31 Julai 2016

BFA YAPATA VIONGOZI WAPYA WA MIAKA MINNE IJAYO

indexMwenyekiti mpya wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Bagamoyo(BFA) Alhaj Abdul Sharif ,wa katikati kati ya waliokaa ,akiwa na viongozi wenzake wa chama hicho ,waliochaguliwa mapema  mwishoni mwa wiki iliyopita.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
indexMwenyekiti mpya wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Bagamoyo(BFA)alhaj Abdul Sharif ,akizungumza na wajumbe wa chama hicho baada ya uchaguzi wa chama hicho ambapo kilipata viongozi wapya watakaoongoza kwa miaka minne ijayo.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
………………………………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
CHAMA cha mpira wa miguu ,wilayani Bagamoyo,mkoa wa Pwani,( BFA) kimechagua viongozi wapya wa chama hicho wataokingoza katika kipindi cha miaka minne .
Uchaguzi huo umefanyika kihalali ,kwa mujibu wa sheria ambao ulihudhuliwa na wajumbe 91.
Katika uchaguzi huo alhaj AbdulZahoro Sharifu alichaguliwa kuwa mwenyekiti kwa kipindi kitakachoishia mwaka 2020 kwa kupata kura 77.
Alhaj Sharif alipata ushindi huo kwa kupata kura hizo dhidi ya mpinzani wake Kitomu Yona aliyepata kura 11 huku nafasi ya makamu mwenyekiti alichaguliwa Shaabani Makelele ambae hakuwa na mpinzani.
Nafasi ya katibu mkuu imenyakuliwa na John Fransis Bolizozo “Boli Kubwa” aliyejipatia kura 81 na kumwacha mbali mgombea mwenzie kwenye nafasi hiyo Yona Mkawa aliyejinyakulia  kura 4.
Katibu msaidizi alishinda Jitihada Omary kwa kura zote kutokana na kuwa peke yake ,mhazini alichaguliwa Ornjurie Marigwa ambae hakuwa na mpinzani  msaidizi ikienda kwa Salumu Kanuti aliyejikusanyia kura 88.
Mjumbe mkutano mkuu wa mkoa alichaguliwa kipa wa zamani wa nyota nyekundu na kocha mzawa hapa nchini Shekhe Abdallah aliyepata kura 45 dhidi ya kura 43 alizopata Mzee Minjoli.
Nafasi ya mwakilishi wa vilabu akichaguliwa Jabir Omary aliyeshinda kwa kura 46 akimwacha mgombea mwenzake Ally Jakaya aliyepata kura 44.
Wajumbe kamati ya utendaji na kura zao katika mabano waliochaguliwa ni Ramadhani Mape (77), Rajabu Maliki (80), Maneno Kidobe (68), Shabani Masimbi (69) na Peter Nyambasi (39).
Katika uchaguzi huo uliongozwa na mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wilaya Mwinyi Akida, mwenyekiti aliyemaliza muda wake Shaabani Kangale “Machokodo” na diwani wa kata ya Kiwangwa Hussein Malota Kwaga.
Baada ya kutangaza matokeo hayo Akida aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanawatumikia ipasavyo wana-Bagamoyo ili mpira uchezwe maeneo yote.
Alieleza kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kukidhi kiu ya wana michezo ambao kwa muda mrefu hususan ukanda wa Chalinze na maeneo mengine wilayani humo ambao wamekosa fursa hiyo.
Nae mwenyekiti mpya wa BFA ,Abdul Sharif, alitoa rai kwa viongozi wengine wa chama hicho kuhakikisha kila mmoja anajitoa kwa hali na mali ili kuinua sekta ya michezo wilayani humo.
Alhaj Sharif aliahidi kupatikana kwa timu itakayocheza ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika kipindi cha miaka minne ambacho watakiongoza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni