SERIKALI YAANZISHA MPANGO MAALUM WA UPIMAJI WA ARDHI MAENEO YASIYOPIMWA JIJINI DAR ES SALAAM.
 Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
……………………………………………………………………………………………….
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
Serikali
 kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeandaa mpango 
maalumu wa upimaji wa Ardhi na Urasimishaji wa maeneo yote yasiyopimwa 
katika jiji la Dar es salaam ambapo viwanja zaidi ya  laki tatu 
(300,000) vitapimwa na wamiliki wake kupewa Hati.
Akizungumza
 leo jijini Dar es salaam kuhusu zoezi hilo, Katibu Mkuu wa Wizara ya 
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Mozes Kusiluka amesema kuwa 
Serikali imeamua kuja na mpango huo kwa sababu ya ukubwa wa jiji hilo na
 wingi wa watu ulioambatana na ujenzi wa makazi holela.
“Katika
 mwaka wa fedha 2016/2017 tumepanga kuwa na mpango maalum wa jiji la Dar
 es salaam ambapo  wataalam wetu watakwenda, kuhakiki mipaka na kupima 
maeneo yote ambayo hayajapimwa na kutengeneza ramani zitakazoonyesha 
maeneo ya barabara na maeneo ya huduma nyingine kwa kushirikiana na 
wananchi husika.
Amesema
 kuwa baada ya zoezi la uhakiki Serikali itatoa hati za maeneo hayo na 
kusisitiza kuwa zoezi hilo litafanyika pia katika maeneo mengine ya miji
 mikubwa nchini yenye watu wengi ikiwemo jiji la Mwanza.
Dkt. 
Kusiluka amesisitiza kuwa urasimishaji utakuwa shirikishi kwa 
kuwahusisha watu wote wa maeneo yatakayopimwa na Serikali ambapo 
wananchi wenye nyumba watashirikiana na viongozi wa Serikali katika 
mitaa kupanga na kuimarisha mindombinu ya maeneo yao pamoja na 
kukubaliana maeneo ambayo barabara za mitaa zitapita, mitaro ya maji 
machafu, magari ya kupitishia huduma za dharula kama Zimamoto nay ale ya
 kubebea wagonjwa.
“Mpango
 wa urasimishaji ni Shirikishi, wataalam wa ardhi watakwenda kwenye 
maeneo yote yatakayopimwa hususan katika jiji la Dar es salaam na kukaa 
na wananchi wote,kupitia mipaka wakishirikiana na wananchi wote kwa 
uwazi ili zoezi hilo liwe na manufaa na tija kwa wananchi wote” 
Amesisitiza Dkt. Kusiluka.
Amesema
 kuwa licha ya kuwepo kwa sheria zinazoisimamia sekta ya Ardhi  nchini 
Tanzania bado sekta hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo 
migogoro ya Wakulima na wafugaji, migogoro ya kijinai ya mtu mm kuvunja 
nyumba au kuvamia eneo la mtu bila idhini, migogoro ya mipaka kati ya 
majirani na ile inayosababishwa na wananchi kutokujua sheria.
Mbali
 na sababu hizo amebainisha kuwa idadi ya watu na matumizi ya ardhi kwa 
shughuli mbalimbali imekuwa ikiongezeka wakati ardhi ikibakia ileile 
jambo linaloifanya sekta hiyo kuja na mikakati mbalimbali ya kukabiliana
 na changamoto hizo kupitia watalaam waliopo.
Amesema
 kuwa serikali imefanya mambo mbalimbali kuhakikisha kuwa inatatua kero 
za wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali kwa kuwatumia wataalam 
wake kupima na kupanga maeneo ya vijiji mbalimbali, kutoa elimu pia 
kuajiri wataalam wa masuala ya Ardhi katika Halmashauri zote nchini.
Aidha amesisitiza kuwa Serikali imejipanga kupima maeneo yote ya ardhi nchini ambayo hayajapimwa kupitia mpango wa miaka 10.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni