NAIBU WAZIRI MPINA AZITAKA RADIO ZA JAMII KUHAMASISHA USAFI WA MAZINGIRA
……………………………………………………………………………………………
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa 
Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb) amezitaka 
Radio za jamii kuhamasisha usafiri wa mazingira nchini. Naibu  Waziri 
Mpina ametoa kauli hiyo alipokuwa akishiriki siku ya usafi kitaifa, 
 mwishoni mwa wiki wilayani Masasi Mkoani Mtwara.
Akitolea Mfano wa Radio Pride FM 
ya Mjini Mtwara yenye kupatikana katika frequencies 87.8 mjini Mtwara, 
ambayo imeanzisha kampeni ya usafi katika mkoa wa mtwara na wilaya zake 
kwa kufanya vipindi vya moja kwa moja na kutembelea wilaya za mkoa huo 
kufanya usafi wa mazingira kwa vitendo.
Kwa Upande wake Bw. JUma Andrea 
Manager uzalishaji wa kituo hicho cha Radio, alisema kuwa lengo kubwa la
 kituo hicho kuhamasiha usafi ni kuunga mkono agizo la Mhe. Rais kwa 
kuwaweka pamoja wananchi, kuweka muamko na hamasa ili kujenga tabia ya 
kupenda usafi na kuepukana na magonjwa yatokanayo na uchafu akitolea 
mfano ugonjwa wa homa ya matumbo na kipindipindu.
Akiongea na Uongozi wa Mkoa wa 
Mtwara katika majumuisho ya ziara yake Wilayani Masasi, Naibu Waziri 
Mpina aliwataka viongozi wa mkoa huo kuunda sheria ndogondogo za 
mazingira zitakazo watoza faini wananchi waharibifu wa mazingira mkoani 
humo, na kuwachukulia hatua za kisheria kulingana na hali ya wananchi 
ili waweze kujifunza na kujijengea tabia ya usafi.
“Nimeona kuwa uchomaji moto 
misitu ovyo hapa kwenu umekithiri, uchomaji moto taka nao siyo njia 
nzuri ya uondoshwaji wa taka,hiyo kuwe na miondombinu rafiki kwa 
uondoshwaji wa taka, na kiongozi wa mkoa ambae hatakuwa tayari 
kushughulikia usafi wa mazingira na yeye awe tayari kushughulikiwa 
alisisitiza.”
Ziara ya Naibu Waziri Mpina 
Mkoani Mtwara ni muendelezo wa Ziara zake nchini za ukaguzi wa viwanda 
na usafi wa mazingira iliyohusisha pia ukaguzi wa machinjio ya mji wa 
Masasi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni