MAKOCHA TANZANIA WAANZA KUIVA
Kidao amesema japo kozi hiyo 
ilikuwa hatua ya kwanza ‘Module 1’ kwa sasa wameiva kiasi kwamba 
watakapomaliza Novemba, mwaka huu wana uhakika wa kupeleka vyeti vyao 
sehemu yoyote duniani kuomba kazi na kushinda kwa kuwa wameiva vilivyo. 
Wakufunzi wa kozi hiyo walitokea CAF, Sunday Kayuni na Salum Madadi 
ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF.
Baada ya kusikiliza kauli hiyo ya
 Kidao, Rais wa TFF Jamal Malinzi moja kwa moja akawasisitiza makocha 
hao kufanya kazi kwa juhudi na kuwaeleza kuwa hatua waliyofikia ni kubwa
 kwa kuwa baadhi ya makocha kutoka nje hawana vyeti na kukosa sifa ya 
kufundisha timu kubwa ikiwamo timu za mataifa ngazi mbalimbali.
Rais Malinzi alitaka makocha hao 
kuangazia mpira wa miguu kwa wavulana wengi wakiwa wanatokea katika 
mashindano yanayodhaminiwa na Kampuni ya simu ya Airtel pamoja na soko 
la wasichana ambalo kwa sasa linashika chati kila kona ya dunia.  
Naye, Makamu wa Rais wa TFF, 
Wallace Karia alimpongeza Rais Malinzi kwa namna anavyoratibu na 
kuzikubali kozi mbalimbali za waamuzi na makocha. “Kwa muda mrefu au 
tuseme kwa miaka mingi hakujafanyika kozi nyingi kama kipindi cha 
uongozi wako ukisaidiana na mimi pamoja na kamati nzima ya utendaji 
pamoja na sekretarieti.”
“Fanyeni utafiti ninyi makocha. 
Utaona kuwa sehemu kubwa nchi za Afrika zimefanikiwa kwa kutumia makocha
 wazawa. Leo ninyi ni makocha wa ngazi ya juu kabisa hivyo mna uwezo wa 
kufanya vema na kusaidia timu zetu na timu za taifa,” alisisitiza Karia.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni