JKCI Yafanya Upasuaji wa Moyo, Mtoto Apandikizwa Betri ya Umeme wa Moyo (peacemaker)
Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)
………………………………………………………………………..
Na John Stephen
Dar es Salaam, Tanzania. Taasisi 
ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)-Muhimbili LEO imefanya upasuaji mkubwa 
wa moyo kwa mtoto, Happiness John Josephat ambaye amepandikizwa 
 peacemaker (betri ya umeme wa moyo) kwenye mfumo wa moyo wake.
Mmoja wa madaktari wa moyo 
walioshiriki kwenye upasuaji huo, Dk Godwin Sharau wa taasisi hiyo 
amesema upasuaji huo umechukua saa moja na kwamba mtoto anaendelea 
vuzuri.
Dk Sharau amesema mtoto huyo 
amepandikizwa peacemaker (betri ya umeme wa moyo) ambayo itasaidia 
kuunganisha mishipa ya fahamu ya umeme wa moyo ambayo inaunganisha 
vyumba vya moyo vya juu na chini kwenye moyo wa binadamu.
“Upasuaji huu ni wa kwanza 
kufanyika Tanzania. Upasuaji kama huu unafanyika kwa watu wazima, lakini
 watu wazima hawahitaji upasuaji wa moyo wa kupandikiza. Watoto 
wanahitaji upasuaji wa moyo wa kuipandikiza.
“Tatizo la mtoto huyu ni la 
kuzaliwa. Na ni nadra kutokea. Inaweza kupita miaka mingi bila watoto 
kutokea tatizo kama hilo. Upasuaji umefanywa kwa ushirikiano wa 
madaktari wa moyo na madaktari wa matibabu ya moyo nikiwamo mimi (Dk. 
Godwin Sharau), Dk Michael Valentine kutoka Marekani,  Dk  Kisenge na Dk
 Sulende Kubhoja, Dk wa usingizi, Dk Anjelan Muhozya na madaktari 
wengine ambao wamesaidia katika upasuaji huu,” amesema Dk Godwin Sharau.
Mama wa mtoto huyo, Elitruda Eligi
 Malley ambaye ni mkazi wa Sakina-Raskazon mkoani Arusha amewashukuru 
madaktari wa Taasisi hiyo kwa kufanya upasuaji huo na mtoto wake kutoka 
salama katika chumba cha upasuaji.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni