NDIKILO :ALILIA USHIRIKIANO NA WIZARA ZA VIWANDA NA ARDHI
SERIKALI
 mkoani Pwani ,imeiomba serikali kupitia wizara ya viwanda,biashara na 
uwekezaji na wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi kushirikiana 
na mkoa huo katika kushughulikia migogoro ya ardhi hasa inayohusisha 
wawekezaji na jamii.
Aidha
 imeitaka wizara ya ardhi kushirikisha wadau mbalimbali wa mkoa katika 
kushughulikia migogoro hiyo ili kuondoa migongano isiyo ya lazima.
Akizungumzia
 juu ya kusuasua kumalizika kwa baadhi ya migogoro ya ardhi inayohusisha
 makundi ya watu na wawekezaji ,mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist 
Ndikilo,alisema katika migogoro ya aina hiyo pande zote zinastahili 
kupewa haki.
Alisema inawapa wakati mgumu iwapo serikali ya mkoa inakuwa na maamuzi yake na wizara ya ardhi kufikia maamuzi mengine.  
Mhandisi
 Ndikilo,alieleza kuwa endapo ikitokea malalamiko yoyote kuhusu 
wawekezaji na jamii wanashauri wizara kuhusisha wadau wengi .
“Wizara
 inawapokea watu hatukatai lakini iangalie kwani kuna makundi mengine ya
 watu ambao wameshaharibu mkoani hapa ambapo wizara pasipo kujua inawapa
 red capet hatimae kukwamisha juhudia za kimaendeleo zinazofanywa na 
serikali ya mkoa”alisema mhandisi Ndikilo.
Mkuu
 huyo wa mkoa alieleza kuwa wizara ya ardhi isiwe nyepesi kukubali 
kufanyia kazi malalamiko ya kuporwa ardhi ,yanayopelekwa kwao na baadhi 
ya wananchi na makundi  yanayovamia mashamba ama maeneo yanayomilikiwa 
na wawekezaji  ambao wengi wao ni wakiukwaji wa sheria.
Mhandisi
 Ndikilo alisema ushahidi walionao kimkoa kutoka katika vyombo vya dola 
baadhi ya wananchi na vikundi hivyo wanauza ardhi na mapato wanayopata 
hayanufaishi serikali za vijiji wala halmashauri husika badala yake 
wananufaisha matumbo yao.
Alisema
 wamekuwa wakijipatia mamilioni ya shilingi kwa kuuza ardhi za watu 
wanaomiliki kihalali na baadae serikali ikiingilia kati wanakimbilia 
wizarani .
“Serikali
 ya mkoa na wilaya wakiwafikisha watu hao katika vyombo husika 
wanakimbilia wizara ya ardhi na kupokelewa na kukwamisha maendeleo 
lakini mkoa utaendelea kuwashughulikia ili kila mmoja apate haki yake 
“alisema mhandisi Ndikilo.
Hata hivyo alisema  tayari alishaandika barua juu ya maombi hayo na namna mkoa ulivyojipanga kuinua sekta ya uwekezaji .
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni