Jumapili, 17 Julai 2016

NDIKILO :ALILIA USHIRIKIANO NA WIZARA ZA VIWANDA NA ARDHI

indexNa Mwamvua Mwinyi,Kibaha
SERIKALI mkoani Pwani ,imeiomba serikali kupitia wizara ya viwanda,biashara na uwekezaji na wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi kushirikiana na mkoa huo katika kushughulikia migogoro ya ardhi hasa inayohusisha wawekezaji na jamii.
Aidha imeitaka wizara ya ardhi kushirikisha wadau mbalimbali wa mkoa katika kushughulikia migogoro hiyo ili kuondoa migongano isiyo ya lazima.
Akizungumzia juu ya kusuasua kumalizika kwa baadhi ya migogoro ya ardhi inayohusisha makundi ya watu na wawekezaji ,mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo,alisema katika migogoro ya aina hiyo pande zote zinastahili kupewa haki.
Alisema inawapa wakati mgumu iwapo serikali ya mkoa inakuwa na maamuzi yake na wizara ya ardhi kufikia maamuzi mengine.  
Mhandisi Ndikilo,alieleza kuwa endapo ikitokea malalamiko yoyote kuhusu wawekezaji na jamii wanashauri wizara kuhusisha wadau wengi .
“Wizara inawapokea watu hatukatai lakini iangalie kwani kuna makundi mengine ya watu ambao wameshaharibu mkoani hapa ambapo wizara pasipo kujua inawapa red capet hatimae kukwamisha juhudia za kimaendeleo zinazofanywa na serikali ya mkoa”alisema mhandisi Ndikilo.
Mkuu huyo wa mkoa alieleza kuwa wizara ya ardhi isiwe nyepesi kukubali kufanyia kazi malalamiko ya kuporwa ardhi ,yanayopelekwa kwao na baadhi ya wananchi na makundi  yanayovamia mashamba ama maeneo yanayomilikiwa na wawekezaji  ambao wengi wao ni wakiukwaji wa sheria.
Mhandisi Ndikilo alisema ushahidi walionao kimkoa kutoka katika vyombo vya dola baadhi ya wananchi na vikundi hivyo wanauza ardhi na mapato wanayopata hayanufaishi serikali za vijiji wala halmashauri husika badala yake wananufaisha matumbo yao.
Alisema wamekuwa wakijipatia mamilioni ya shilingi kwa kuuza ardhi za watu wanaomiliki kihalali na baadae serikali ikiingilia kati wanakimbilia wizarani .
“Serikali ya mkoa na wilaya wakiwafikisha watu hao katika vyombo husika wanakimbilia wizara ya ardhi na kupokelewa na kukwamisha maendeleo lakini mkoa utaendelea kuwashughulikia ili kila mmoja apate haki yake “alisema mhandisi Ndikilo.
Hata hivyo alisema  tayari alishaandika barua juu ya maombi hayo na namna mkoa ulivyojipanga kuinua sekta ya uwekezaji .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni