KONGAMANO LA VIJANA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI MKOANI MWANZA LAFANYA.
Mgeni
 Rasmi, Meneja wa Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo SIDO mkoani 
Mwanza, Damian John Changa, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Biashara,
 Viwanda na Uwekezaji, katika ufungaji wa Kongamano la Vijana 
Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza lililohitimishwa jana katika 
Viwanja vya Gandh Hall Jijini Mwanza. 
Alisema
 umefika wakati wa vijana kuacha kuilalamikia Serikali huku wakiwa 
hawajishughulishi katika kujipatia kipato hivyo kongamano hilo anaamini 
limewafungua vijana wengi mkoani Mwanza ambao watatumia elimu ya 
ujasiriamali na uwekezaji waliyoipata kutumia fursa zilizopo mkoani 
Mwanza ili kujikomboa kiuchumi.
Kongamano
 hilo lilifanyika kwa siku mbili kuanzia jumamosi Julai 16,2016 hadi 
jana jumapili julai 17,2016 ambapo liliandaliwa na Taasisi ya Tanzania 
Youth Enterpreurship Organization pamoja na Taasisi ya Vijana Mwanza 
Saccos kwa lengo la kuwawezesha vijana kukutana pamoja kuzungumza, 
kujadili na kutathimini kwa pamoja fursa zilizopo mkoani Mwanza na 
kuzitumia ili kukabiliana na changamoto za kiuchumi.
Kauli mbiu ya Kongamano hilo ilikuwa ni “Kijana ndio Mhimili wa Upaishaji wa Pato la Taifa, Usisubiri kesho, Fursa ni Sasa”.
Afisa
 Maendeleo ya Jamii Jijini Mwanza, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi 
wa Jiji la Mwanza, katika hitimisho la Kongamano la Vijana Wajasiriamali
 na Wawekezaji mkoani Mwanza.
Mwenyekiti
 wa Kongamano la Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza, 
akizungumza katika hitimisho la kongamano hilo jana.
Alisema
 kongamano hilo limevunga lengo la kuwafikia vijana 1,100 kwani zaidi ya
 vijana 2,000 walihudhuria huku pia lengo la kuvifikia vikundi 50 vya 
wajasiriamali mkoani Mwanza likivukwa baada ya vikundi 150 kujiandikisha
 na kushiriki katika kongamano hilo.
Beatus Kisusi ambae alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Kongamano hilo akizungumza wakati wa ufungaji wake jana.
Florah
 Magabe ambae alikuwa mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano la 
Vijana Wawekezaji na Wajasiriamali mkoani Mwanza, alitanabaisha kwamba 
lengo ni kongamano hilo kufanyika katika mikoa mbalimbali nchini ili 
kuwafikia vijana wengi zaidi ili waweze kutumia fursa zilizopo katika 
kujikwamua kiuchumi.
Mdau
 wa Maendeleo Jijini Mwanza ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kahama 
Mjini, Jumanne Kishimba, akitoa Mada kuhusu “Watu waliopambana na Maisha
 na kufanikiwa katika harakati za kuzalisha mali”.
Mh.Dkt.Antony
 Diallo ambae ni Mkurugenzi wa Sahara Media Group, akitoa mada juu ya 
“Ujasiriamali na Uwekezaji katika Mkoa wa Mwanza” katika kongamano la 
Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza.
Miongoni mwa watoa Mada katika kongamano hilo ambae alitoa mada juu ya “Umuhimu wa Bima katika Biashara”.
Kulwa
 William Matolwa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano TCRA Kanda ya Ziwa, 
akitoa mada katika kongamano hilo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mamlaka 
hilo Kanda ya Ziwa.
George Binagi-GB Pazzo ambae ni blogger wa BMG, akitoa mada juu ya Matumizi yakinifu ya Mitandao ya Kijamii na Biashara.
Jummy
 Peter Masumbuko ambae ni Mratibu Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na 
Ufugaji wa Viumbe Maji kutoka Taasisi ya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya 
Uvuvi mkoani Mwanza-FETA akitoa mada katika kongamano hilo
Maneno Abubakary kutoka SIDO mkoani Mwanza, akitoa mada katika kongamano hilo.
Donald Kasongi ambae ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Governance Links, akitoa mada katika kongamano hilo.
Mwalimu Beny Mwenda kutoka Chuo cha UKIRIGURU mkoani Mwanza, akitoa mada katika kongamano hilo.
Mwenyekiti
 wa Taasisi ya The Desk and Chair Foundation, Sibtain Meghji, akitoa 
salamu za taasisi hiyo ambayo ilifadhiri kwa asilimia kubwa kongamano 
hilo ambapo alisisitiza kwamba makongamano ya aina hiyo kufanyika mara 
kwa mara ili kusaidia kuwapatia vijana elimu ya ujasiriamali na 
uwekezaji huku akisisitiza zaidi pia fursa za makongamano na maonyesho 
kama ya Sabasaba pia kufanyika mikoani badala ya kusalia tu Dar es 
salaam.
Baadhi
 ya waliohudhuria kongamano hilo akiwemo Mwenyekiti wa Machinga Jijini 
Mwanza, Masanja Matondo (kushoto), wakifuatilia matukio kwa umakini 
zaidi
Baadhi ya wadau wakifuatilia Kongamano hilo akiwemo Katibu wa Machinga Jijini Mwanza (kushoto).
Burudani live kutoka kwa Ramyy Ramulla a.k.a Katoto Ka Mama Rama.
Atrey Kuni ambae ni Afisa Habari, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, aliongoza vyema Kongamano hilo.
Wadau katika picha ya pamoja
Mgeni
 Rasmi (wa tano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Waandaaji wa 
Kongamano la Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza.
Tazama Hapa Picha za Ufunguzi wa Kongamano Hil
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni