INFANTINO AMSIFU MALINZI
Rais
wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Gianni Infantino
amemsifu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuwa ni
miongoni mwa viongozi wa vyama vya soka duniani walioamua kuendesha soka
kwa weledi kutokana na kuratibu mafunzo mbalimbali kwa makocha na
waamuzi.
Salamu
za Infantino zimetolewa na Msimamizi Mkuu wa kozi ya waamuzi nchini,
Carlos Henrique kutoka Afrika Kusini akisema, “Infantino ana ripoti zote
ya namna mpira wa miguu unavyoendeshwa duniani. Anasifu Tanzania kwa
namna mnavyopiga hatua. Ana ripoti idadi ya makocha walivyokuwa wachache
na sasa mna makocha wengine wako kwenye kozi.
“Mbali
ya makocha, leo tuko nanyi waamuzi, ni hatua kubwa ambayo Rais
Infantino amemsifu Rais wa TFF, Bwana Malinzi,” alisema Henrique.
Henrigue
aliyeka waamuzi hao kujikita zaidi kusoma namna sheria 17 za mpira wa
miguu zilivyoboreshwa kwa kuondoa zaidi ya maneno 1,000 ili kuja
kusimamia vema michezo wa soka huku akiwataka kuwa mahiri wakati wote.
Henrique anafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na Mark Mzengo kutoka
Malawi, Felix Tangawarima wa Zimbabwe na Gladys Onyago kutoka Kenya.
Kozi
za Waamuzi wa Mpira wa Miguu wa Tanzania sasa ilianza jana Julai 25,
2016 kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa
(FIFA) na waaamuzi waandamizi wanaotarajiwa kuveshwa beji hizo kwa
majina yao kupendekezwa FIFA kama watapata matokeo mazuri kwenye kozi
inayoendelea.
Kozi
ilianza kwa ratiba ya waamuzi wote kuchukuliwa vipimo (physical fitness
test) kwa kila mwamuzi chini ya wakufunzi hao kutoka FIFA. Baada ya
vipimo, darasa la waamuzi hao litaanza kwa nadharia na vitendo. Darasa
hilo litafikia mwisho Julai 29, 2016 kabla ya kuanza darasa la waamuzi
wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya
StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo
kwa msimu wa 2016/2017.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni